WAZIRI MKUU AFAFANUA KUHUSU KUTENGULIWA KWA UTEUZI WA WAZIRI KITWANGA

WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amesema uamuzi wa Rais Dk. John Pombe Magufuli kutengua uteuzi wa Waziri wa Mambo ya Ndani, Bw. Charles Kitwanga umefuata kanuni za utumishi wa umma ambao unakataza mtumishi kulewa akiwa kazini. 
“Zipo sheria za utumishi ambazo mtumishi hatakiwi kunywa pombe na wala hapaswi kulewa akiwa kazini… mtumishi anapaswa kuwa na akili timamu inayokuwezesha kufanya kazi za Serikali,” alisema.                                                   
Ametoa ufafanuzi leo usiku (Ijumaa, Mei 20, 2016) wakati akijibu swali la mwandishi wa TBC1aliyetaka kujua kama taarifa zilizoenea kuhusu kutenguliwa kwa Waziri huyo ni za kweli. 
“Ni kweli Mheshimiwa Rais, Dk. John Pombe Magufuli ametengua uteuzi wa Waziri wa Mambo ya Ndani, Mheshimiwa Charles Kitwanga kuanzia leo tarehe 20 Mei, 2016 baada ya kuonekana amelewa wakati wa kazi. Na hili lilibainika pale alipokuwa akijibu maswali ya wizara yake leo asubuhi,” alisema Waziri Mkuu. 
Waziri Mkuu amesema kuna swali aliloulizwa ambalo hakulijibu vizuri na kwamba swali hilo litapaswa kurudiwa kuulizwa baada ya wabunge kuomba muongozo wa swali hilo.

IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU,
S. L. P. 980,
DODOMA.
IJUMAA, MEI 20, 2016.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 16 mpaka sasa

  1. Chemical engineer ame dectect fume ya alcohol,Hii aibu kubwa.....heri katumbua....

    ReplyDelete
  2. AnonymousMay 20, 2016

    uamuzi sahihi kwa wakati sahihi. sasa tufahamu uhusika wake LUGUMI na wabia wake wabanwe mapema kabisa.

    ReplyDelete
  3. AnonymousMay 20, 2016

    Ni kama vile golikipa kajifunga mwenyewe goli, ili mradi wapinzani wasionekane kuwa washindi.Lakini ukweli uko pale pale, bao ni bao la penati na hata la kujifunga wenyewe..mmeshafungwa. alex bura dar

    ReplyDelete
  4. AnonymousMay 20, 2016

    Je alikuwa ananuka pombe, au hatakuongea hawezi? walimfanyiavipimokuona alikuwa na kiasi gani cha pombe kwenye damu? kweli hapa ni kasi ya kazi tu. Hapendwi mtu hapa, na hakuna maroroso.

    ReplyDelete
  5. it is very shameful sikio la kufa halisikii dawa atafutiwe kazi anayofanana naye

    ReplyDelete
  6. AnonymousMay 20, 2016

    Is this a case of Auto-brewery syndrome? when affected individuals auto ferment Alcohol in their gut, with the help of one of the gut`s yeast known as saccharomyces cerevisiae. If this is not the case and he really consumed alcohol before going to the parliament, then he has reaped what he sowed!
    Dr G.Bitozi

    ReplyDelete
  7. AnonymousMay 21, 2016

    Dr Bitozi andika basi hata kizungu kinachoeleweka. Ama nawe uko under the influence ama ni ubitozi tu?

    ReplyDelete
  8. AnonymousMay 21, 2016

    Ahhhh wapi..........hahahaha mwaka huu wengi tu watafundishwa kulewa ili kuuficha ukweli, watu walikomaa mpaka kikaeleweka na bado mjipange kweli kweli.

    ReplyDelete
  9. AnonymousMay 21, 2016

    Pole sana Mh. Kitwanga.Yote ni maisha, aliyekupa ni huyo huyo kakunyakuwa kama ni Mungu au JPM.au Tekero.
    Labda umelogwa! Maana kwa akili ya kawaida hii haiingi akilini( can"t complihend what you did)Kwa kitendo hicho umemsaliti JPM, wana Misungwi, wanaCCM wote, watumishi wa wizara ya mambo ya ndani, na watanzania wa vyama vyote wapendao maendeleo.
    Kwa maisha bora nakuomba uchukuwe rozari seriously na uanze kusali ili kilichomo ndani yako kiondoke. Ni Bwana tu ndiye awezae yote, maana kama ni vita basi ni vyake.
    Ankal Michuzi chonde! chonde! nakuomba utuwekee wimbo wa Dr. Remmy uitwao 'NISEME NINI" maana una mafunzo makubwa na ya ziada kwetu sisi tuliobakia.

    ReplyDelete
  10. AnonymousMay 21, 2016

    Help him. Apelekwe Rehab.

    ReplyDelete
  11. AnonymousMay 21, 2016

    ULEVI NI MAMA WA MAASI NA UTOVU WA NIDHAMU.
    ULIMWENGU UNGEKUWA VINGINE KABISA SIKU ULEVI UNGEPIGWA MARUFUKU. OTHERWISE MENGI KAMA HILI TUTAENDELEA KUYASHUHUDIA. ALCOHOL HAS NEVER BEEN MAN'S BEST FRIEND...
    AND IT NEVER WILL BE!!
    Mndengereko Ukerewe

    ReplyDelete
  12. AnonymousMay 21, 2016

    Jamani uthibitisho kuwa alikuwa amelewa upo? Ukweli taarifa hii haijakaa vizuri, ni kama kadharirishwa!

    ReplyDelete
  13. AnonymousMay 21, 2016

    Njamumanyilezu@gmail.com

    ReplyDelete
  14. AnonymousMay 21, 2016

    How can we verify on the truth kwamba alikuwa amelewa?

    ReplyDelete
  15. AnonymousMay 21, 2016

    I think now Ministers now for sure know who is their boss!..... but let us wait and see if they are terrified enough to execute their duties responsibly.

    ReplyDelete
  16. Ni sawa...lkn hapa CCM ndio ninapowaona kiboko.....wameepusha LUGUMI kwa kuua Issue kwa KIROBA. ..kweli CCM KIBOKO..

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...