Na Zainab Nyamka, Globu ya Jamii.
BAADA ya kumalizika kwa hatua ya 16 bora ya kombe la Shirikisho na kufanikiwa kupatikana kwa timu 8 zilizoingia kwenye makundi hatimaye Droo ya kupanga timu hizo inafanyika Jumanne ya Mei 24.
Shirikisho la mpira wa miguu Aftika (CAF) limeamua kupanga ratiba hiyo na hatua ya makundi itaanza kupigwa Juni 17.
Wajumbe wa kamati ya Mashindano watakutana Jumatatu Jijini Cairo nchini Misri makao makuu ya CAF ili kuweza kufanya mchakato wa kuandaa taratibu za kupanga makundi katika timu 8 ili kuweza kujua timu gani zinakaa pamoja.
Timu zilizofanikiwa kuingia Young African (Tanzania) , TP Mazembe ( DRC) , Etoile Du Sahel ( Tunisia),
3 Mo Bejaia (Algeria), Madeama (Ghana), Kawkab Marrakech (Morocco), Al Ahly Tripoli (Libya) ,Fus Rabat (Morocco).



Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...