JESHI LA ULINZI LA WANANCHI WA TANZANIA
KURUGENZI YA HABARI NA UHUSIANO

Simu ya Upepo   : “N G O M E”                Makao Makuu ya Jeshi,
Simu ya Mdomo : DSM  22150463            Sanduku la Posta 9203,
Telex                     : 41051                           DAR ES SALAAM,21  Mei, 2016
Tele Fax                : 2153426
Barua pepe       : ulinzimagazine@yahoo.co.uk
Tovuti                  : www.tpdf.mil.tz

Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania linapenda kutoa taarifa ya ufunguzi wa mashindano ya kombe la Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi (CDF CUP) ambayo yanatarajiwa kufunguliwa rasmi tarehe 24 Mei 2016 katika uwanja wa Uhuru jijini Dar es salaam. Mgeni rasmi katika ufunguzi huo anatarajiwa kuwa Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Mhe. Nape Nnauye.
 Mashindano haya yalianzishwa mwaka 2014, awali JWTZ lilikuwa likiteua wanamichezo wa kushiriki michezo ya kimataifa kupitia timu teule za Jeshi hali iliyopelekea kutovumbuliwa kwa vipaji vipya katika michezo, ikaonekana upo umuhimu wa kubadili mfumo wa uteuzi. Hivyo kuanzisha mashindano ya Kombe la  Mkuu wa Majeshi (CDF CUP) ambayo huanzia ngazi za vikosi hadi kufikia ngazi za brigedi.
lengo la mashindano haya ni kudumisha mshikamano, kuvumbua na kukuza vipaji, pia mashindano hayo yatatumika katika kuteua kombaini ya timu ya JWTZ itakayoliwakilisha Jeshi na Taifa kwa ujumla katika mashindano ya michezo ya majeshi na utamaduni kwa nchi za Jumuiya ya Afrika Mashariki yanayotarajiwa kufanyika nchini Rwanda mwezi wa nane mwaka huu.
Kauli Mbiu ya mashindano haya ni “Michezo ni Ulinzi na Umoja Daima”
Timu zinazoshiriki mashindano haya ni Ngome (Makao Makuu JWTZ), Kamandi ya Jeshi la nchi kavu ikiwakilishwa na timu za Tembo, Faru, Nyuki, Mbuni na Chui, Kamandi ya Jeshi la Anga, Kamandi ya Jeshi la Wanamaji pamoja na Jeshi la Kujenga Taifa(JKT).
Mashindano haya yatahusisha michezo ifuatayo, Mpira wa miguu kwa wanaume, Mpira wa kikapu kwa  wanaume, Mpira wa mikono kwa wanaume, Mpira wa pete kwa wanawake na Mbio za nyika kwa wanaume na wanawake.Michezo hii itafanyika katika viwanja vya Twalipo vilivyopo Mgulani pamoja na uwanja wa Uhuru jijini Dar es salaam. 
Mashindano haya yanatarajiwa kufungwa rasmi tarehe 06 Juni 2016. Mgeni rasmi katika ufungwaji wa mashindano haya anatarajiwa kuwa Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi Tanzania Jenerali Davis Mwamunyange.

Wananchi wote wanakaribishwa. Hakuna kiingilio.
  
Imetolewa  na  Kurugenzi  ya  Habari  na  Uhusiano
Makao Makuu ya Jeshi, Upanga
S.L.P  9203,   Dar es Salaam,  Tanzania.

Kwa Mawasiliano zaidi: 0756716085/ 0713506757

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

  1. AnonymousMay 21, 2016

    Ni aibu kubwa kwa jeshi la ulinzi wa nchi yetu kutuimia anwani ya baruapepe ya yahoo.co.uk/ ambayo ni ya bure na huku likiwa na tovuti yake kamili.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...