KATIKA  harakati za kuhabarisha jamii  kwa maranyingine EFM redio imeleta mapinduzi kwa kufanya vipindi vyote  moja kwa moja kutoka mtaani kwako  leo, kuanzia kipindi cha Joto la asubuhi kinachorushwa kuanzia saa 12:00 - hadi Saa 3:00 asubuhi, pamoja na  vipindi vyote kama sports .

Headquarters, Uhondo, Ladha 3600, na kumalizia  na kipindi cha Ubaonikwa kushirikisha wakazi wa mtaa husika pamoja na kujadili mambo kadha wa kadha kuhusiana na kero, changamoto, kwa lengo la kuwaleta karibu wasikilizaji wake.
Mbali na vipindi hivyo pia kuna burudani kutoka kwa wasanii wa singeli kama M-cizo, Young Yuda, Majid Migoma, Easy Man, pamoja na Sholo Mwamba.
 Wakazi wa wilaya ya Temeke wakisikiliza matangazo ya moja kwa moja  katika viwanja hivyo vya mwembeyanga-Tandika.
 Matangazo yalianza moja kwa moja katika kipindi cha joto la asubuhi kushoto ni Gerald Hando, Adela Tillya pamoja na Paul James (PJ).
  Watangazaji wa kipindi cha Sports Headquarters Kutoka kushoto ni Ibrahim Masoud (Maestro), Maulid Kitenge , Omari Katanga, wengine ni Musa Mwakisu, Yusuphu Mkule pamoja na Osca Oscar.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...