Gulio la simu Expo litakalofanyika katika viwanja vya posta Kijitonyama jijini Dar es Salaam kesho Jumamosi na Jumapili wiki hii litawawezesha wateja wa Vodacom Tanzania na wananchi kwa ujumla kujipatia simu za uhakika zenye gharama nafuu ikiwemo simu za bure kwa wateja watakaonunua vifurushi vya aina mbalimbali vya muda wa maongezi na intanenti.
Akiongea juu ya gulio hilo,Mkurugenzi Mkuu wa Mawasiliano na Uhusiano wa Vodacom Tanzania,Rosalynn Mworia alisema kuwa lengo la gulio hili ni kuwawezesha wateja wa kampuni kuweza kupata maelezo kuhusu huduma za kampuni ikiwemo kuweza kununua simu halisi zenye viwango vinavyotakiwa kwa gharama nafuu kuanzia simu za shilingi elfu 18/- na kuna ofa ya wateja kujipatia simu za bure kabisa.
“Gulio hili la Vodacom Simu Expo limekuja katika wakati mwaafaka ambapo tarehe ya mwisho ya kuzima simu zisizo na viwango inakaribia hivyo tunawakaribisha wateja wetu wote watembelee gulio hilo na kuweza kujipatia simu zenye viwango vinavyostahili kwa gharama nafuu ambapo pia watapata fursa ya kupata maelezo ya huduma zetu mbalimbali” Alisema.
Alisema katika gulio hilo pia kutakuwepo na watoa huduma mbalimbali ambao watashughulikia matatizo ya simu za mkononi pamoja na huduma zinginezo kwa wateja watakafika kwenye gulio hilo.
SOMA ZAIDI HAPA
SOMA ZAIDI HAPA
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...