Chama cha mchezo wa kuogelea nchini (TSA) kimeipongeza klabu ya Dar Swim Club (DSC) kwa kufanya semina ya kuendeleza mchezo huo kwa wachezaji na makocha iliyokuwa chini ya wakufunzi kutoka klabu ya Hamilton Aquatics ya Dubai.

Pongezi hizo zimetolewa na Katibu Mkuu wa TSA, Ramadhan Namkoveka mara baada ya kutembelea mafunzo hayo yaliyofanyika kwenye bwawa la kuogelea la shule ya kimataifa ya DIA iliyopo Masaki jijini.

Mafunzo hayo yalikuwa chini ya wakufunzi wa kimataifa wa mchezo wa kuogelea wa klabu bingwa ya Mashariki ya Kati (Middle East) ijulikanayo kwa jina la Hamilton Aquatics ya Dubai, Nebojsa Durkin na Katy Morris.

Mafunzo hayo yalidhaminiwa na kampuni za Alios Finance Tanzania, Europcar, DSC, DIA na kampuni ya utafiti na uchimbaji wa mafuta ya Maurel & Prom.

Wakufunzi hao walifuraishwa na viwango vya waogeleaji wa klabu hiyo pamoja na kukabiliana na changamoto mbalimbali za mchezo huo ikiwa pamoja na kukosa bwawa la mita 50 linalotambuliwa kimataifa.

Namkoveka alisema kuwa wamefuraishwa na mafunzo hayo ambayo yaliwahusisha waogeleaji chipukizi (yoso) na wakubwa pia na makocha wa timu hiyo. Alisema kuwa wamevutiwa na jinsi mafunzo hayo yalivyokuwa yanaendeshwa na anaamini Tanzania itapata waogeleaji nyota kama wadau wa mchezo huo wataiga mfano wa DSC.
Kocha wa timu ya DarSwim Club, Radhia Gereza (kulia) na Salum Mapunda (kushoto) wakiwaelekeza waogeaji watoto wa klabu ya Dar Swim Club baada ya kupata mafunzo kutoka kwa wakufunzi wa klabu ya Hamiton Aquatics ya Dubai.

“Nimefuraishwa na jinsi mafunzo yalivyoendeshwa, kwa kweli nimevutiwa sana kwani nimeona jinsi waogeleaji chipukizi waliokuwa wanaanza kujifunza mchezo, waogeleaji wenye uelewa wa mchezo na makocha walivyokuwa wanapewa mafunzo, hii ndiyo njia sahihi ya kuendeleza mchezo huu,”

BOFYA HAPA KUSOMA ZAIDI

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...