Mtaalam kutoka Idara ya Nishati, Wizara ya Nishati na Madini, Mhandisi Marwa Petro (kushoto) akielezea majukumu ya Wizara mbele ya Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini anayeshughulikia Nishati, Dkt. Juliana Pallangyo (wa pili kutoka kulia, mbele) mara Naibu Katibu Mkuu alipotembelea banda la Wizara kwenye Maonesho ya  Kimataifa ya  Sabasaba yanayoendelea katika  viwanja vya Mwalimu Nyerere jijini  Dar es Salaam.
 Mtaalam kutoka Shirika la Umeme Nchini (TANESCO) Mhandisi Musa Chowo (kushoto) akieleza gridi ya Taifa inavyofanya kazi kwa Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini anayeshughulikia Nishati, Dkt. Juliana Pallangyo ( wa pili kutoka kushoto)
 Mtaalam kutoka  Wakala wa Ukaguzi wa Madini Nchini (TMAA) Mhandisi Yisambi Shiwa (kulia) akieleza jinsi  shughuli za ukaguzi wa madini zinavyofanyika nchini kwa Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini anayeshughulikia Nishati, Dkt. Juliana Pallangyo ( wa kwanza kushoto) mara alipotembelea banda la TMAA.
 Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini anayeshughulikia Nishati, Dkt. Juliana Pallangyo (katikati) akioneshwa jinsi majiko yanayotumia nishati mbadala yanavyofanya kazi na Afisa Masoko kutoka  Kampuni ya Envotec Services Limited Salama Sudi (kulia) ambao ni mdau wa Wakala wa Nishati  Vijijini (REA).


Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...