Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Prof. Makame Mbarawa akitoa maelekezo kwa Maafisa Uhamiaji katika Kiwanja cha Ndege Cha Kimataifa Cha Julius Nyerere(Terminal II), alipotembelea kuangalia utendaji kazi na vifaa vya Mamlaka hiyo jijini Dar es Salaam.
 Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Prof. Makame Mbarawa, akitoa malekezo wa Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Tanzania (TAA) Mhandisi George Sambali (Katikati), alipotembelea Mamlaka hiyo.
 Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Prof. Makame Mbarawa, akitoa malekezo wa Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Tanzania (TAA) Mhandisi George Sambali (Katikati), alipotembelea Mamlaka hiyo.
                                                   (Picha na Benjamin Sawe- Maelezo)
WAZIRI MBARAWA AIAGIZA TAA KUONGEZA MAPATO.
Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Prof. Makame Mbarawa ameiagiza Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Tanzania (TAA) kuongeza kiwango cha ukusanyaji mapato kutoka Bilioni 74 hadi kufikia bilioni 105 katika mwaka wa fedha 2016/2017.

Ametoa agizo hilo jijini Dar es Salaam wakati akizungumza na wafanyakazi wa Mamlaka hiyo mara baada ya kukagua majengo matatu na ofisi mbalimbali zilizopo Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Mwl. Julius Nyerere (JNIA).
Amesisistiza wafanyakazi wa Uwanja huo kuhakikisha kiasi cha ukusanyaji wa mapato hayo kinaongezeka siku hadi siku ili kukuza uchumi wa taifa na kuchochea fursa za kimaendeleo.
                                                        KWA PICHA ZAIDI BOFYA HAPA.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...