Waziri wa Katiba na Sheria, Dk Harrison Mwakyembe akizungumza na viongozi wa Kampuni ya Uchimbaji Madini ya mkoani Geita (GGM) pamoja na Viongozi wa Serikali wa mkoa huo, kuhusiana na masuala mbalimbali ya utatuaji wa migogoro iliyopo kati ya GGM na wananchi wanaoishi jirani na mgodi huo. Waziri Mwakyembe aliambatana na Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni, katika ziara hiyo.
Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni akizungumza jambo katika kikao chao na Mkuu wa Mkoa wa Geita, Meja Jenerali Mstaafu Ezekiel Kyunga (katikati), na Waziri wa Katiba na Sheria, Dk Harrison Mwakyembe (wa tatu kushoto) mara baada ya kuwasili mkoani humo kwa ajili ya ziara ya kikazi zilizofanywa na viongozi hao wa Wizara. Wapili kushoto ni Mkurugenzi wa Mashtaka (DPP), Biswalo Mganga.
Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Uchimbaji Madini ya Geita (GGM), Terry MulPeter akizungumza katika kikao kati ya uongozi wa kampuni yake na viongozi wa serikali uliokuwa unaongozwa na Waziri wa Katiba na Sheria, Dk Harrison Mwakyembe na Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni (hawapo pichani). Kikao hicho kilifanyika katika Ukumbi wa Mikutano wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Geita.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...