KIASI cha Dola za Marekani bilioni moja kimetengwa kwa ajili ya kuimarisha zao la muhogo nchini kupitia mkataba wa kibiashara baina ya Serikali ya Tanzania na kampuni ya Tanzania Agricultural Export Processing Zone Limited and Epoch Agriculture (TAEPZ) kutoka China.
Akizungumza wakati wa utiaji saini makubaliano hayo jijini Dar es Salaam mwishoni mwa wiki, Katibu Mkuu Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji anayeshughulikia viwanda Dk. Adelhelm Meru, alisema huu ni wakati wa wakulima kunufaika na Kilimo cha muhogo baada ya kulima kimazoea.
Alisema, kwa muda mrefu Watanzania wamekua wakilima muhogo kwa ajili ya chakula tu huku wakisafirisha muhogo ghafi hali inayokosesha serikali mapato na kunufaisha mataifa ya nje kupitia zao hilo lenye manufaa mengi.
“Lengo la serikali kuwa na uchumi wa viwanda linaanza kutimia, huu ni uwekezaji mkubwa katika sekta ya kilimo cha biashara. Kutakuwa na shamba kubwa la mihogo, kutajengwa viwanda mbalimbali vya kuzalisha unga wa mihogo, makopa, chakula cha mifugo, sukari ya viwandani na mbolea.
“Hii fursa tusiiache, kama mlikua mkilima mihogo kwa kiwango kidogo ongezeni mashamba kwa sababu soko la uhakika lipo, pia tunashauri mnunue hisa katika kampuni hii ili ikiwezekana tuimiliki kwa kiwango kikubwa,” alisema Dk. Meru.
Katibu Mkuu Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji anayeshughulikia viwanda Dk. Adelhelm Meru (kushoto), akiwa na Mwenyekiti wa TAEPZ, Dior Feng wakati wa kutia saini makubaliano ya mradi wa zao la muhogo nchini utakaogharimu Dola za Marekani bilioni 1. Waliosimama kutoka kushoto ni balozi wa China nchini, Dk. Lu Youqing na Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Sekta Binafsi Nchini (TPSF), Godfrey Simbeye. Mwishoni mwa wiki jijini Dar es Salaam.
Katibu Mkuu Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji anayeshughulikia viwanda Dk. Adelhelm Meru (kushoto), akibadilishana nyaraka na Mwenyekiti wa TAEPZ, Dior Feng baada ya kusaini mradi wa zao la muhogo nchini utakaogharimu Dola za Marekani bilioni 1. Wanaoshuhudia kutoka kushoto ni balozi wa China nchini, Dk. Lu Youqing na Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Sekta Binafsi Nchini (TPSF), Godfrey Simbeye. Mwishoni mwa wiki jijini Dar es Salaam.
Katibu Mkuu Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji anayeshughulikia viwanda Dk. Adelhelm Meru, akizungumza katika hafla ya utiaji saini makubaliano ya mradi wa kusindika muhogo nchini utakaogharimu Dola za Marekani bilioni 1, wengine katika picha ni Mwenyekiti wa TAEPZ, Dior Feng na Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Sekta Binafsi Nchini (TPSF), Godfrey Simbeye. Mwishoni mwa wiki jijini Dar es Salaam.


Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...