WAKULIMA wa viazi Mkoani Njombe wameushukuru Mpango wa kuendeleza Kilimo Ukanda wa kusini mwa Tanzania (SAGCOT) kwa kuwaletea mradi wa uzalishaji na usambazaji mbegu bora za viazi pamoja elimu juu ya zao hilo ambapo sasa uzalishaji wake umeongezeka.
Wakizungumza kwa nyakati tofauti, wakulima wa viazi mkoani hapa wamewaambia waandishi habari jana kuwa kuwepo kwa mradi huu toka SAGCOT umetusaidia kutoka katika kilimo cha mazoea na kuingia kwenye kilimo biashara.
Mchungaji Michael Nyagawa toka kijiji cha Lunguya, kata ya Mtwango Halmashauri ya Wilaya ya Njombe ni mmoja wa wakulima waliofaidika na mradi wa uzalishaji na usambazaji wa mbegu bora za viazi toka SAGCOT alisema wakulima wa viazi walikuwa na mazingira magumu katika uzalishaji.
“Tulifika kipindi hekali moja ya viazi unavuna gunia 20 tu, lakini sasa tunapata gunia 60 mpaka 80 kwa hekali,” alisema MchungajiNyagawa na kufafanua kuwa kupitia mafunzo na mbegu mpya toka SAGCOT uzalishaji wa viazi umeongezeka na kuinua vipato kwa wakulima,” alisema.
Mchungaji huyo hakusita kusema kuwa kutokuwa na elimu ya kutosha kuhusu zao hilo vilichangia uzalishaji kuwa mdogo kama vile uandaaji wa shamba, namna ya kupanda mbegu, uhifadhi wa mbegu katika maghala na pia mbegu ilikuwa ya zamani sana.
“SAGCOT imetupatia mbegu za aina nne ambazo ni Tengeru,Sherekea,Asante na Meru ambazo zimetolewa bure kwa sisi wakulima” alisema Mchungaji Nyagawa na kuongezea kuwa hata pale tunapovuna mazao yote yanakuwa mali yetu.
Mtaalam na Mratibu wa Mradi wa kuzalisha na kusambaza mbegu bora za viazi mviringo kwa wakulima – Njombe toka SAGCOT, Bw.Owekisha Kwigizile akitoa mafunzo kwa wanakikundi cha Matunda group katika kata ya Mhaji, halmashauri ya Wilaya ya wanging’ombe Mkoani Njombe hivi karibu alipowatembelea na kuwaelimisha juu y Mradi wa kuzalisha na kusambaza mbegu bora za viazi mviringo unaoratibiwa na Mpango wa kuendeleza kilimo ukanda wa kusini mwa Tanzania (SAGCOT). Chini ya unafadhiliwa na Serikali ya watu wa Marekani(USAID) kupitia Shirika la Kimataifa la kusimamia mapinduzi ya kijani barani Afrika(AGRA).
Mkulima Bi Sara Martin akimwonesha kitu Mtaalam na Mratibu wa Mradi wa kuzalisha na kusambaza mbegu bora za viazi mviringo kwa wakulima – Njombe toka SAGCOT, Bw.Owekisha Kwigizile alimpomtembelea shambani kwake katika kijiji cha Maduma kata ya Kichiwa ,Halmashauri ya wilaya ya Njombe na kuona maendeleo ya kilimo cha zao hilo. Mradi huo unafadhiliwa na Serikali ya watu wa Marekani(USAID) kupitia Shirika la Kimataifa la kusimamia mapinduzi ya kijani barani Afrika(AGRA)na kuratibiwa na Mpango wa kuendeleza kilimo ukanda wa kusini mwa Tanzania(SAGCOT).
Mkulima Bi. Agusta Madembwe wa kijiji cha Nyanga, kata ya Ikuna, Halmashauri ya wilaya ya Njombe akikagua shamba lake alilipanda mbegu mpya za viazi mviringo alizozipata kupitia Mradi wa kuzalisha na kusambaza mbegu bora za viazi mviringo kwa wakulima – Njombe unaoratibiwa na Mpango wa kuendeleza kilimo ukanda wa kusini mwa Tanzania (SAGCOT). Akiwa na matumaini makubwa ya uzalishaji kwani amelima kwa njia ya kisasa.


Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...