
Mkurugenzi
Mtendaji wa Makampuni ya Mohammed Enterprises Tanzania Limited (MeTL
Group), Mohammed Dewji amekanusha taarifa ambazo zimesambaa katika
mitandao mbalimbali ya kijamii kuwa amefanya mahojiano na kituo cha
Redio cha Times FM kuhusu pesa zilizochangishwa katika Tetemeko la Ardhi
la Kagera lililotokea mwezi Septemba, 2016.
Dewji amesema hajafanya mahojiano na kituo chochote cha habari kuhusu tetemeko la Kagera na habari hiyo haina ukweli wowote zaidi ni mbinu ambayo imetumiwa na baadhi ya watu kwa ajili ya kuchafua jina lake na kampuni yake ya MeTL Group ambayo mpaka sasa ina wafanyakazi zaidi ya watu 28,000.
Aidha Dewji amesema ana imani na Serikali ya awamu ya tano na kuwatoa hofu Watanzania kuwa ataendelea kushirikiana na Serikali kusaidia jamii yenye uhitaji ikiwa ni sehemu ya ahadi yake ya kutumia nusu ya utajiri wake kusaidia watu wenye uhitaji.
“Nitumie nafasi hii kuwajulisha Watanzania wenzangu kuwa hii habari ambayo inasambazwa na watu katika mitandao ni ya uongo na haina ukweli wowote, sijafanya mazungumzo na media yoyote na mimi nilichangia pesa kwa nia nzuri, nina imani na Serikali ya awamu ya tano inayoongozwa na Rais Dk. John Magufuli kuwa inafanya kazi kwa faida ya watu wote bila kufanya ubaguzi,” amesema Dewji.
Katika ujumbe ambao unaonekana kusambaa katika mitandao mbalimbali ya kijamii ikiwepo Facebook, Instagram na WhatsApp imeandikwa kuwa MO Dewji amefanya mahojiano na Redio Times FM na kusema kama angejua mapema kuwa wahanga hawatopatiwa pesa hizo asingechangia


Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...