JAMHURI
YA MUUNGANO WA TANZANIA
WIZARA
YA NISHATI NA MADINI
UTOAJI RUZUKU AWAMU
YA TATU KWA WACHIMBAJI MADINI WADOGO, TAREHE 17 JANUARI 2017, MPANDA.
Serikali kupitia Wizara ya Nishati na
Madini, kwa kushirikiana na Benki ya Dunia (WB) itatoa Ruzuku ya jumla ya Shilingi
Bilioni 7.481 kwa Wachimbaji Madini Wadogo 59
waliokidhi vigezo vya kupata ruzuku hiyo kati ya 592 walioshindanishwa.
Hafla ya utoaji wa Ruzuku
hiyo itafanyika siku ya Jumanne, tarehe 17 Januari 2017, Mjini Mpanda katika
Uwanja wa Shule ya Msingi,
KASHAULILI.
Mgeni Rasmi atakuwa
Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Kassim M. Majaliwa
(Mb.).
Taarifa
zaidi kuhusu Ruzuku hiyo inapatikana
katika Tovuti ya Wizara ya Nishati na Madini, www.mem.go.tz
na Ofisi za Madini za Kanda.
Imetolewa
na,
Prof. Justin W. Ntalikwa
KATIBU MKUU



Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...