Mufti Mkuu wa Tanzania Sheikh Aboubakar Zubeiry akizungumza mapema leo jijini Dar es salaam katika hafla ya uzinduzi wa huduma mpya kutoka Zantel iliyopewa jina la ‘Zantel Madrasa’ ambayo ni mahususi kwa waumini wa dini ya Kiislamu kujifunza imani ya dini hiyo pamoja na kupata mafundisho kupitia simu za mkononi ambapo kwa watumiaji wa mtandao wa Zantel watakaopenda kutumia huduma hii watatakiwa kupiga simu au kutuma ujumbe mfupi kwenda namba 15586 na kufuata maelekezo. (katikati) ni Mkurugenzi Mkuu wa Zantel, Benoit Janin na Mkuu wa kitengo cha huduma na bidhaa Zantel Hamza Zuheri.

 Mkurugenzi Mkuu wa Zantel, Benoit Janin akizungumza leo jijini Dar es salaam katika hafla ya uzinduzi wa huduma mpya kutoka Zantel iliyopewa jina la ‘Zantel Madrasa’ ambayo itawawezesha waumini wa dini ya Kiislamu kujifunza kuhusu imani ya dini hiyo pamoja na kupata mafundisho kupitia simu zao za mkononi. (Katikati) ni Mufti Mkuu wa Tanzania Sheikh Aboubakar Zubeiry ambaye alikuwa mgeni rasmi na Mkuu wa Itifaki BAKWATA Mohammed Nassor.
 Mufti Mkuu wa Tanzania Sheikh Aboubakar Zubeiry na Mkurugenzi Mkuu wa Zantel Benoit Janin wakionyesha vipeperushi vya huduma mpya ya ‘Zantel Madrasa’ kuashiria uzinduzi rasmi wa huduma hiyo uliofanyika mapema leo jijini Dar es salaam.

BOFYA HAPA KWA PICHA ZAIDI

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...