Na Mwandishi Wetu, Globu ya Jamii
VIONGOZI wa kamati ya Utendaji wa Yanga wakutana leo kujadili masuala mbalimbali ya klabu hiyo kutokana na kuwa katika hali ngumu ya ukata inayoikabili.
Kutoka ndani, kikao huo ulioanza toka asubuhi kimekuwa cha siri sana wakiwa katika majadiliano makali na pia ikionekana kutaka kuinusuru klabu hiyo kutoka kwenye hali hiyo ambapo imepoteza mchezo wa Jumamosi dhidi ya Simba.
Kamati ya Utendaji wa Yanga wameamua kukutana leo ikiwa ni siku mbili baada ya Katibu Mkuu wa Yanga Boniface Mkwasa kuweka wazi hali ya ukata wa klabu hiyo, pia wachezaji kulalamika kuhusiana na kutokulipwa mishahara yao.
Pia, kumekuwa na taarifa kuwa mchezaji wa kimataifa kutokea nchini Zimbambwe kuweka wazi kuwa baadhi ya viongozi walidanganywa kuwa anaweza kucheza katika mechi dhidi ya Simba wakati si kweli.



Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...