Na Karama Kenyunko, Blogu ya jamii.
MFANYABIASHARA wa Kariakoo, Casto Onyomolile Ngogo (35) amepandishwa kizimbani katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu kujibu mashtaka ya kukutwa na sare mbalimbali za Jeshi la Wananchi Tanzania JWTZ.

Mshtakiwa huyo ambaye amesomewa mashtaka yake mbele ya Hakimu Mkazi Thomas Simba anashtakiwa chini ya sheria ya uhujumu uchumi.

Akisoma hati ya mashtaka, Wakili wa Serikali, Wankyo Simon amedai Juni 15, 2017 mshtakiwa huyo anayeishi Tabata Segerea, alikutwa na Suruali 5000 za JWTZ zenye thamani ya milioni 50.

Mshtakiwa huyo anadaiwa kukutwa na vifaa hivyo katika maeneo ya bandari kavu ya Galco Inland Container (ICD) iliyopo Sokota Chang'ombe.

Pia mshtakiwa huyo alikutwa na alikutwa na maofisa wa polisi akiwa na tisheti 50 za JWTZ zenye thamani ya Sh 500, 000 pia Juni 17, mwaka huu huko African Inland Container Deport mshtakiwa alikutwa na polisi akiwa na pea 20 za viatu vya JWTZ bila ya kuwa na uhalali.

Mshtakiwa huyo hakuruhusiwa kujibu kitu chochote kwa sababu mahakama hiyo haina mamlaka kusikiliza kesi hiyo hadi Mahakama Kuu.
Pia (DPP) amewasilisha hati ya kuzuia dhamana chini ya kifungu cha 36 (2) cha sheria ya uhujumu uchumi. Kesi imeahirishwa hadi Agosti 29,mwaka huu.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...