Klabu ya Simba inawatangazia waandishi wote wa habari za michezo,kuwa kesho siku ya Jumatatu 18/9/2017 kutakuwa na mkutano.
Mkutano huo utafanyika kwenye ukumbi mdogo wa klabu kuanzia majira ya saa 6 mchana, pamoja na mengine yatakayozungumzwa hiyo kesho,mkutano huu ni muhimu sana kwako/kwenu kuhudhuria kwani kuna mengi ya umuhimu ya kuyatolea ufafanuzi na kuyaweka wazi kwa umma wa mashabiki na wanachama wetu kupikia kwako/kwenu.
Tunasisitiza kuwahi,kwani mkutano huo utaanza katika muda uliotajwa hapo juu na utazingatia muda.
Mwisho Klabu inapenda kuwapa taarifa rasmi,kuwa kuanzia sasa kila siku ya Jumatatu tu tutakuwa na mkutano na nyinyi/wewe kuanzia majira ya saa 6 mchana kwenye ukumbi wa klabu,hivyo basi ni vyema mkaiongeza ratiba hii kwenye ratiba zenu za kazi za kila siku.
Imetolewa na Mkuu wa kitengo cha habari na mawasiliano
Haji Sunday Manara.
Simba Nguvu Moja..!!!
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...