WASANII na wanamichezo mbali mbali nchini, wameendelea kujiunga na kundi Uzalendo Kwanza lenye nia ya kuurudisha uzalendo wa Mtanzania.
Akizungumza jiji jana, Mwenyekiti wa Kampeni ya Uzalendo Kwanza Steve Nyerere alisema wasanii hao wapya na wanamichezo watatambulishwa rasmi kesho.
"Kipindi cha kampeni za uchaguzi kama taifa tuligawanyika, wapo waliokuwa CCM na wapo waliokuwa Ukawa, ni muda muafaka sasa kuacha tofauti zetu za itikadi na kumuunga mkono muheshimiwa rais." alisema Nyerere
Nyerere alisema kampeni ya 'Uzalendo kwanza' ambayo itafanyika mikoa mbali mbali itaenda sambamba na kutoa misaada kwa jamii.
Kampeni hiyo ilizinduliwa hivi karibuni inalengo la kuhamasisha wananchi, taasisi na mashirika mbali mbali kuunga mkono juhudi za Rais John Pombe Magufuli katika jitihada za kuleta maendeleo, ikiwa ni pamoja na kuwa wazalendo kwa kulinda rasilimali za nchi.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...