Baadhi ya waandishi wa Habari kutoka vyombo mbalimbali vya Habari zikiwemo Televisheni na Magazeti
Jana walitembelea vituo vya Usajili mkoa wa Arusha kuona hatua za usajili na mwitikio wa wananchi
katika kupata haki yao msingi ya kikatiba ya kusajiliwa.
Wananchi wa Mkoa wa Arusha wameendelea kujitokeza kwa wingi kujisajili Vitambulisho vya
Taifa; huku idadi ya Kata za Usajili zikiongezeka. Moja ya Kata iliyoanza Usajili jana kwa upande
wa Wilaya ya Arusha mjini inaendelea kuwasajili wananchi katika Kata ya Themi, Sekei,
Sombetini na wameongeza Kata nyingine ya Sinoni.
Wilaya ya Monduli inakamilisha usajili kwenye Kata za Monduli Mjini, Monduli Juu na Engutoto;
ikijipanga kuendelea na Kata za Lashaine, Sepeko, Meserani na Mfereji. Kwa Upande wa
Arumeru Kata zinazofanya Usajili ni Musa, Ambureni, Leburuki, Imbasenyi na Ngabobo, Longido
ni Kata za Olubomba, Namanga na Kimokoa na wanajiandaa na Kata za Kamwanga, Tingatinga,
Olumorodi na Sinya. Karatu wanaendelea na Usajili kwenye Kata ya Karatu na Rhotia kabla ya
kuhamia Ganako. Wilaya ya Ngorongoro wameanza na Tarafa ya Ngorongoro kabla ya kuanza
Mitijo.
Uongozi wa Mkoa umejizatiti kuhakikisha wananchi wote wanasajiliwa kwa wakati na kupata
Vitambulisho vya Taifa vitakavyowawezesha kushiriki katika shughuli mbalimbali za uzalishaji
mali pamoja na upatikanaji kirahisi wa huduma za kijamii.
Kaimu Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano (NIDA) Bi. Rose Joseph (mwenye
miwani) akizungumza na baadhi ya waandishi wa Vyombo vya Habari vya Televisheni
na Magazeti walipotembelea kituo cha usajili cha Sombetini, Arusha mjini kuangalia
shughuli za kuwasajili wananchi zinazoendelea kituoni hapo.
Wananchi wakiendelea kupata huduma za usajili kabla ya kupigwa picha
kama wanavyoonekana pichani. Wananchi hao ambao ni kutoka Kata ya Sombetini
wamekuwa wakijaziwa fomu na kugongewa mihuri na wenyeviti kwenye mitaa
wanayoishi kabla ya kusajiliwa kwenye mfumo wa NIDA.
Mwenyekiti wa mojawapo ya mitaa ya Kata ya Sombetini (mwenye
kofia) akigonga mhuri kwenye fomu ya mwananchi kuthibitisha kumtabua, na mkazi wa
eneo lake.
Akina mama pamoja na jukumu la malezi wamejitokeza kusajiliwa kama
anavyoonekana pichani mmoja wa akinamama wa Kata ya Sinoni akiwa amembeba
mtoto wake mkono mmoja na mkono mwingine akiwa anaendelea na hatua za
usajiliwa. Kwa habari zaidi BOFYA HAPA
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...