NA TIGANYA VINCENT-RS –TABORA

JUMLA ya wakulima 4,268 wilayani Urambo wamejiandikisha kulima zao la Pamba katika msimu wa kilimo unatarajia kuanza wakati wowote mwezi huu.

Kauli hiyo imetolewa jana na Mkuu wa Wilaya ya Urambo Angelina Kwingwa wakati akitoa taarifa ya maandalizi ya kilimo hocho kwenye ziara ya Mkuu wa Mkoa wa Tabora Aggrey ambaye anazungukia vijiji mbalimbali vinavyolima pamba kwa ajili ya utoaji wa elimu juu ya ulimaji bora.Alisema kuwa idadi ya wakulima wanatoka Kata 15 ambao wamo katika vijiji 49 wameleta makisio yao ya kulima zao hilo na kuongeza wakifanikiwa kulima zinaweza kupatika zaidi tani 2000.

Kwingwa alisema kuwa maandalizi yanakwenda vizuri ambapo wanatarajia kupata mbegu ambazo zimependekezwa na Bodi ya Pamba zisizokuwa na Manyoa tani 31.2 kwa ajili ya kusambaza kwa wakulima kwa ajili ya kuanza kilimo hicho.Naye Mkuu wa Mkoa wa Tabora Mwanri aliwaonya wakulima na wafanyabiashara kutoingiza mbegu za manyoya ambazo zimepigwa marufuku na kuongeza kuwa mkulima atakayepanda mbegu hizo atalazika kuzing’oa.

“Hapa mbegu tutakayopanda ni UKM08 na sio nyingine …nikikutana mtu amepanda mbegu iliyopigwa marufuku ya manyoa nitavuruga shamba lake na kuwachukulia hatua watu ambao watakuwa wamebainika kuingiza mbegu hiyo” alisisitiza Mwanri.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...