NA K-VIS
BLOG/Khalfan Said
ULE
msemo wa kiswahili wa "mgeni njoo mwenyeji apone", unaweza kutumika
kufatsiri neema ambayo taifa limepata kufuatia ziara ya siku mbili nchini ya
Kamishna wa Jumuiya ya Umoja wa Ulaya (EU) anayeshughulikia mahusiano ya Kimataifa
na Maendeleo, Mhe. Neven Mimica, pichani juu.
Mhe.
Mimica alianza ziara yake Novemba 2, kwa kutiliana saini makubaliano na
Serikali kupitia Wizara ya Fedha na Mjpango, ambapo EU imeahidi kutoa kiasi cha
Euro milioni 50 ambazo zitatumika kupeleka umeme vijijini.
Serikali
inapambana kuhakikisha vijiji elfu 12 (12,000) ambavyo bado havina umeme nchini
vinapata huduma ya umeme ifikapo 2020.Kwa
mujibub wa Afisa Habari wa EU hapa nchini Bi.Susanne Mbise, msaada huo wa Euro
milioni 50 utasaidia kupeleka umeme kwenye vijiji 3,000.
Ziara ya
Kamishna Mimica, ililenga kutembelea shughuli mbalimbali ambazo EU imekuwa
ikifadhili,
Miongoni
mwa maeneo ambayo Kamishna Mimica alitembelea ni pamoja na bandari ya Dar es
Salaam, ambapo akiongea na uongozi wa bandari hiyo, Kamishna Mimica a,lieleza
utayari wa EU katika kusaidia kub oresha bandari hiyo kwani ina msada mkubwa
sio tu kwa Tanzania bali pia kwa nchi majirani.
Kamishna
Mimica pia ametembelea kituo kinachosaidia vijana cha Nafasi Art Space kilichoko
Mikocheni jijini Dar es Salaam ambapo aliweza kusikiliza maoni yao na
kujadiliana nao masuala mbalimbali yahusuyo changamoto za ajira na pia ukatili
dhidi ya mtoto wa kike. "Kamishna Mimica amesema EU itatoa Euro milioni 500 ili kusaidia kupambana na ukatili
dhidi ya wanawake na watoto". amesema Bi. Mbise.
Kamishna
huyo wa EU, alikutana na kujadiliana na makampuni makubwa ya kibinafsi ili
kuona jinsi sekta binafsi inavyofanya shughuli zake hapa nchini na ziara hiyo
ilimuwezesha pia kukutana na viongozi wa asasi za kiraia hapa nchini.
Kamishna wa Jumuiya ya Umoja wa Ulaya (EU) anayeshughulikia mahusiano ya Kimataifa na Maendeleo, Mhe. Neven Mimica, (kushoto), akiwa na balozi wa EU nchini, Mhe.Roeland van der Geer, wakati amkizungumza na waandishi wa habari kwenye ukumbi wa Makumbusho ya Taifa jijini Dar es Salaam, mwishoni mwa ziara yake ya siku mbili nchini Novemba 3, 2017.(PICHA NA HABARI/K-VIS BLOG;Khalfan Said)
Mhe.
Mimica, akipokewa na Kaimu Mkurugezni Mkuu wa Mamlaka ya Bandari
Tanzania, (TPA), Bw. Lazaro twange, alipotembelea bandari ya Dar es
Salaam, Novemba 3, 2017. EU ni mdau mkubwa katika kjuisaidia TPA
kuimarisha miundombinu yake.
Mhe. Mimica akizun gumza na uongozi wa juu wa TPA.
Mhe.
Mimica akipeana mikono na Katibu Mkuu Wizara ya Fedha na Mipango, Mhe.
Dotto James, baada ya kusaini makubaliano ambapo EU itatoa Euro milioni
50 kusaidia usambazaji umeme vijijini. Takriban vijiji 3,000 kote nchini
vitafaidika na msaada huo. Serikali inapambana kuwafikishia umeme wana
vijiji wa vijiji 12,000 a,mbavyo bado havijapata umeme na mpango huu
umepangwa kukamilika 2020.
KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA
KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...