VIONGOZI wa mpira wa miguu katika kata mbalimbali wilayani Handeni, mkoani Tanga, wameaswa kuhakikisha kwamba wanatimiza wajibu wao wa kuratibu na kuyasimamia mashindano ya Ligi ya Handeni Kwetu Cup kwenye Kata zao ili mashindano hayo yawe na tija na kupatikana washindi kwa wakati kama ilivyokusudiwa.

Ushauri huo umetolewa na muasisi wa mashindano hayo, Kambi Mbwana, alipokuwa akizungumza na gazeti hili wilayani hapa, akisema kuwa kuna baadhi ya Kata zimekuwa zikisua sua kutokana na viongozi waliochaguliwa kutojua umuhimu wa uwajibikaji na kutimiza wajibu kwa maslahi mapana ya mpira wa miguu kwa kupitia mashindano hayo yanayodhaminiwa na bahati nasibu ya Biko 'ijue nguvu ya buku' na Mfuko wa hifadhi ya jamii (NSSF).

Akizungumzia suala hilo, Mbwana alisema kabla ya kuanza mashindano hayo, Chama cha Mpira wa miguu wilayani Handeni mkoani Tanga (HDFA), kilichagua viongozi wake kila kata ili pamoja na kuyaratibu mashindano ya Handeni Kwetu kwenye Kata zao kwa ajili ya kutafuta washindi wawili wa kwenda ngazi ya tarafa, pia viongozi hao wangekuwa na majukumu ya kusimamia na kuendeza mpira kwenye kata zao, viongozi ambao upatikanaji wao ulilazimika kutumika kwa gharama ya muda na fedha.

"Kila mdau wa michezo anapaswa kujua kwenye kata yake kuna viongozi wa mpira waliochaguliwa ili kusimamia ligi hii, hivyo wanapaswa kutimiza wajibu wao ili mashindano yetu yaende vizuri kwa ajili ya kutoka kwenye kata na kuingia kwenye tarafa na baadae ngazi ya wilaya kama matarajio yetu.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...