Na Bashir Yakub.

Nakala ya hukumu ya mahakama huhitajika pale kesi au shauri linapokuwa limefika mwisho. 

Kwa lugha nyingine maamuzi ya mahakama ndiyo hukumu ya mahakama. Hapa ndipo tunapojua nani ameshinda na nani ameshindwa. 

Nani anastahili kulipwa au kukabidhiwa mali fulani na nani hastahili. Kadhalika nani anastahili kufungwa na nani anastahili kuachiwa huru. Yote haya na mengine mengi ndiyo yanayojenga kitu kinachoitwa hukumu.

1.UMUHIMU WA NAKALA YA HUKUMU. 

Mara nyingi wale ambao hawakuridhishwa na maamuzi ya mahakama kwenye hukumu hutaka kukata rufaa. Rufaa ni malalamiko yanayopelekwa mahakama ya juu zaidi yakilalamikia hukumu au maamuzi yaliyotolewa na mahakama ya chini. Rufaa hufunguliwa na mtu ambaye hakuridhika na kile kilichoamuliwa. Kwahiyo hata wewe kama unayo kesi ambayo tayari imetolewa hukumu na hukuridhishwa na kile kilichoamuliwa basi unayo haki ya msingi ya kukata rufaa.

Na huna haja ya kuhofu kama unazo sababu za msingi na za kisheria. Waweza kuwa umeshindwa mahakama ya chini lakini ukaibuka mshindi mahakama ya juu ambako umekata rufaa.

Hata hivyo, huwezi kukata rufaa bila kuwa na nakala ya hukumu. Na hapa ndipo linapojitokeza suala la kupata nakala ya hukumu kwa wakati na bila kucheleweshwa. Narudia huwezi kukata rufaa ikiwa hujapata nakala ya hukumu kutoka mahakama iliyotoa uamuzi.

                KUSOMA  ZAIDI  sheriayakub.blogspot.com 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...