Katika kusherehekea siku ya Wafanyakazi Duniani, wafanyakazi wa Ofisi ya Waziri Mkuu wameungana na wafanyakazi wote Duniani kwa kujumuika na wafanyakazi wengine wa hapa nchini jijini Dodoma na kuahidi kuendelea kutoa huduma kwa ufanisi kwa Watanzania.
Wakiongea kwa nyakati tofauti wakati wa sherehe hizo wafanyakazi hao, wamesema kuwa ofisi ya Waziri Mkuu kama mratibu wa shughuli zote za serikali nchini na kama mratibu wa shughuli za Kazi na ajira nchini wataendelea kutekeleza majikumu hayo kwa uadilifu na ufanisi ili huduma zinazotolewa na serkali ziwe zenye tija kwa Watanzania.
Ofisi ya Waziri Mkuu pamoja na kuratibu Shughuli zote za serikali ndani na nje ya Bunge pia inaratibu masuala mtambuka, kama shughuliza maafa, Udhibiti wa matumizi ya madawa ya Kulevya, Vita dhidi ya UKIMWI, Huduma kwa watu wenye Ulemavu. Aidha inahusika na kuchapa nyaraka za uendesheshaji shughuli za serikali, masuala ya Vyama vya siasa, Masuala ya Uchaguzi, Masuala ya kazi, Ajira na maendeleo ya vijana, pamoja na masuala ya uwekezaji na uwezeshaji wananchi kiuchumi.
Maadhimisho ya sherehe za siku ya Wafanyakazi Duniani mwaka huu zimebebwana kauli mbiu ya “Uunganishaji wa Mifuko ya Jamii ulenge kuboresha mafao ya mfanyakazi”
Baadhi ya Wafanyakazi wa Ofisi ya Waziri Mkuu wakipita katika viunga vya jiji la Dodoma kuelekea katika uwanja wa mpira wa miguu wa Jamhuri kushiriki seherehe za siku ya Wafanyakazi Duniani, leo tarehe 1 Mei, 2018.
Baadhi ya Wafanyakazi wa Ofisi ya Waziri Mkuu wakishiriki maandamano ya kuelekea katika uwanja wa mpira wa miguu wa Jamhuri kushiriki seherehe za siku ya Wafanyakazi Duniani, leo tarehe 1 Mei, 2018, Jijini Dodoma.
Wafanyakazi wa Ofisi ya Waziri Mkuu wakipita mbele ya mgeni rasm wakati wa sherehe za siku ya Wafanyakazi Duniani zilizofanyika katika uwanja wa mpira wa Jamhuri Jijini Dodoma tarehe 1 Mei, 2018.
Baadhi ya Wafanyakazi wa Ofisi ya Waziri Mkuu wakifuatilia sherehe za siku ya wafanyakazi Duniani katika uwanja wa mpira wa miguu wa Jamhuri leo tarehe 1 Mei, 2018, Jijini Dodoma.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...