Mganga Mkuu wa mkoa wa Kilimanjaro, Dk. Best Magoma akitoa shukrani kwa Mkuu wa idara ya masoko na mawasiliano wa Benki ya Exim Tanzania kwenye halfa ya makabidhiano ya vitanda na magodoro 50 kwa hospital ya mkoa wa Kilimanjaro ya Mawenzi kama sehemu ya mradi  wa benki hiyo ya miaka 20 ya kujali jamii.
Mkuu wa idara ya masoko na mwasiliano wa benki ya Exim Tanzania, Stanley Kafu  akiongea katika halfa ya makabidhiano ya vitanda na magodoro 50 kwa hospital ya mkoa wa Kilimanjaro ya Mawenzi kama sehemu ya mradi wa benki hiyo ya miaka 20 ya kujali jamii.

  BENKI ya Exim Tanzania leo imekabidhi vitanda na magodoro 50 kwa Hospitali ya mkoa ya Mawenzi, mkoani Kilimanjaro. Benki ya Exim Tanzania iliadhimisha miaka 20 ya huduma, mwezi wa Agosti mwaka jana, kwa kuzindua mradi wa mwaka mzima unaoitwa “miaka 20 ya kujali jamii” ambao Benki hiyo itawekeza katika sekta ya afya Tanzania hasa kwenye kuboresha huduma za afya zinazotolewa kwa wakina mama na wanawake.
Hospitali na kliniki nyingi nchini zina tatizo la ukosefu wa dawa, vifaa na vitanda hasa katika hospitali za rufaa. Katika kukabiliana na uhaba huu unaosumbua taifa, benki ya Exim Tanzania, yenye uwepo wa kimataifa imeanzisha mradi unaolenga kusaidia upungufu wa vitanda katika wodi za wazazi kwenye hospitali nchini - hivyo benki ya Exim itatoa magodoro and vitanda 500 katika hospitali za serikali katika mikoa 13 nchini kama sehemu ya kampeni yake ya mwaka yenye lengo la kusherehekea miaka 20 ya kutumikia jamii.

Hospitali ya Mawenzi mkoani Kilimanjaro ni hospitali ya kumi na moja kupokea mchango huu baada ya hospitali ya serikali ya Sekou Toure ya mkoani Mwanza mwezi uliopita, hospitali ya rufaa ya Morogoro mwezi Aprili, hospitali ya rufaa ya Mwananyamala mkoani Dar es Salaam mwezi Machi, hospitali  ya rufaa ya Bombo, mkoani Tanga mwezi Febuari, hospitali ya rufaa ya Mkoa wa Mbeya mwezi Januari, hospitali ya Mount Meru, Arusha mwezi Desemba, Hospital ya rufaa Dodoma mwezi Novemba, hospitali ya rufaa Ligula, Mtwara mwezi Oktoba, Hospitali ya Mnazi Mmoja, Unguja, Zanzibar mwezi Septemba na Hospitali ya rufaa Temeke, Dar es Salaam mwezi wa nane mwaka jana. Tukio lilifanyika kwenye hospitali hiyo katika wodi ya wazazi na mgeni rasmi alikuwa Mganga Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro, Dr. Best Magoma. 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...