
Dk.
Bashiru ametoa agizo hilo kwa mfanya biashara huyo jana alipokuwa
akizungumza na viongozi wa Chama Cha Mapinduzi na Jumuiya zake katika
Kata ya Nakutupola jijini hapa.Amesema amefikia
uamuzi huo kwa sababu mfanyabiashara huyo ameonekana kutokuwa na
uaminifu wa kutosha kwa kuwa hivi karibuni alizungumza nae ofisini kwake
na kuahidi kukutana ili kufanya makabidhiano ya eneo hilo kwa sherehe
na nderemo kwenye kikao hicho.
"Cha kushangaza
juzi akikuja mwenyewe ofisini kwangu tukaxungumza kwa muda wa saa mbili
tukakubaliana leo aje kwenye kikao hiki kukabidhi eneo letu kwa sherehe
na ndelemo lakini leo nimempigia hadi simu akasema eti ameenda Dar es
Salaam kushughulika na masuala ya mwanae, sasa endeleeni na mazungumzo
na utaratibu wa makabidhiano akabidhi kwa hiari eneo letu", alisema Dk
Bashiru
Dk.
Bashiru aliwataka wanachama na viongozi wa CCM kutofanya vurugu za aina
yoyote kwa Mfanya biashara huyo na kusema Mchakato uliotumika kurejesha
ukumbi ndio utakaotumika kurejesha eneo lote la Chama na mali yote
iliyopo kwenye eneo la hilo ni mali ya CCM.
Katika
mkutano huo Katibu Mkuu wa CCM Dk Bashiru Ally amewapokea Winston
Edward Katibu Kata hiyo wa CUF na Baraka Tayara Katibu kata wa Chadema
pamoja na wanachama 181 kutoka vyama hivyo.
Katibu
Mkuu wa CCM Dkt. Bashiru Ally akipokelewa na Viongozi mbali mbali
alipowasili kata ya Makutupola wilaya ya Dodoma mjini jana
Katibu Mkuu wa CCM Dkt Bashiru Ally akiwapungia Mkono kikundi cha ngoma
Katibu Mkuu wa CCM Dkt Bashiru Ally akizungumza na Viongozi na wanachama wa CCM na Jumuiya zake wa Kata ya Makutupola jana.
HABARI ZAIDI BOFYA HAPA



HABARI ZAIDI BOFYA HAPA
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...