SHIRIKA
la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO) wamekabidhi
rasmi kijiji cha digitali cha Ololosokwan katika sherehe kubwa
iliyofanyika kijijini hapo na kuhudhuriwa na viongozi wa serikali na
mashirika ya Umoja wa Mataifa.
Katika kukabidhiana huko Unesco imesema kwamba itaendelea kutoa msaada katika mtandao wa intaneti kwa miezi sita ijayo.
Katika
hotuba yake iliyosomwa kwa niaba na Dk. Abdul Rahman Lamin, Ofisa
msimamizi wa ofisi ya Unesco, Ann Therese Ndong-Jatta alisema kwamba
wakati wanakabidhi facility hizo wamefurahishwa na ushirikiano mkubwa
waliopewa katika mradi huo.
Kijiji
cha digitali cha Ololosokwan ni moja ya vijiji vinne ambavyo
vimefadhiliwa huku vikitoa huduma muhimu za elimu, afya na biashara
kuendeshwa kidigitali.Kijiji
hicho cha digitali ambacho ni matokeo ya ushirikiano kati ya UNESCO na
kampuni ya Samsung imelenga kutoa elimu kwa kutumia njia ya mtandao,
kufaniklisha tiba mtandao na pia kutumia mtandao wa kompyuta katika
kuwezesha biashara.
Ofisa
huyo alisema kuna haja ya kuendeleza ushirikiano uliopo ili mradi uweze
kuendelea kuchangia maendeleo ya wakazi wa eneo hilo.
Aidha
aliitaka serikali kuhakikisha kwamba inaendeleza ushawishi kwa wananchi
wa eneo hilo la Ngorongoro kutumia vyema teknolojia ya kisasa katika
kufanikisha maisha endelevu ya zana zilizopo.
Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Mh. Mrisho Gambo akizungumza na wananachi wa kijiji cha Ololosokwan pamoja na wageni waalikwa (hawapo pichani) wakati wa hafla ya Unesco kukabidhi kijiji cha digitali cha Ololosokwan kwa serikali, wilayani Ngorongoro mkoani Arusha.
Mwakilishi
wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO)
Abudl Rahman Lamin (wa tatu kushoto) akimwakilisha Ann Therese Ndong’
Jatta, Mkurugenzi wa UNESCO kanda ya Afrika Mashariki akimkabidhi rasmi
ripoti ya mradi wa kijiji cha kidigitali (Unesco-Samsung Digital
Village) kwa Mkuu wa Wilaya ya Ngorongoro, Mh. Rashid Mfaume Taka (wa
tatu kulia) kwa ajili ya uendelezaji baada ya majaribio wakati wa hafla
iliyofanyika katika kituo cha mafunzo ya kazi za mikono na utamaduni cha
jamii ya wamasai (Community Arts Space-CAS) kilichojengwa na Umoja wa
Ulaya (EU) kwa ushirikiano wa Unesco kwenye kijiji cha Ololosokwan
wilayani Ngorongoro mkoani Arusha.
Wengine wanaoshuhudia tukio hilo ni Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Mh. Mrisho Gambo Naibu Katibu Mkuu Elimu wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, Bi. Avemaria Semakafu (waliosimama kwa nyuma), Kaimu Mkuu wa Ofisi za Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO) nchini, Faith Shayo (kushoto), Kaimu Katibu Mkuu wa Tume ya Taifa wa UNESCO nchini Tanzania, Dkt. Moshi Kimizi (wa pili kushoto), Diwani wa kata ya Ololosokwan, Mh. Yannick Ndoinyo (wa pili kulia) pamoja na Mwenyekiti wa Kitongoji cha Ololosokwan, John Pyando (kulia).
Wengine wanaoshuhudia tukio hilo ni Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Mh. Mrisho Gambo Naibu Katibu Mkuu Elimu wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, Bi. Avemaria Semakafu (waliosimama kwa nyuma), Kaimu Mkuu wa Ofisi za Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO) nchini, Faith Shayo (kushoto), Kaimu Katibu Mkuu wa Tume ya Taifa wa UNESCO nchini Tanzania, Dkt. Moshi Kimizi (wa pili kushoto), Diwani wa kata ya Ololosokwan, Mh. Yannick Ndoinyo (wa pili kulia) pamoja na Mwenyekiti wa Kitongoji cha Ololosokwan, John Pyando (kulia).
Baadhi ya wanakijiji wa Ololosokwan waliohudhuria hafla ya Unesco kukabidhi kijiji cha digitali cha Ololosokwan kwa serikali iliyofanyika katika kijiji cha Ololosokwan, wilayani Ngorongoro mkoani Arusha.
HABARI ZAIDI BOFYA HAPA
HABARI ZAIDI BOFYA HAPA
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...