Na Cathbert Kajuna-Kajunason/MMG.

Waziri wa Maji na Umwagiliaji Eng. Isack Kamwelwe ametengua uteuzi wa aliyekuA kaimu Afisa Mtendaji Mkuu wa DAWASA Eng. Romanus Mwang'ingo na kuvunja bodi ya wakurugenzi wa DAWASA.

Akizungumza na waandishi wa Habari jijini Dar es Salaam Eng. Kamwelwe amesema hatua hiyo imechukuliwa ili kupisha uchunguzi wa taarifa ya kuwepo kwa udanganyifu na ubadhirifu katika utekelezaji wa mradi wa kuchimba visima vya maji Kimbiji na Mpera huko Kigamboni jijini Dar es Salaam. 

"Wakati jambo hilo linafanyiwa uchunguzi na TAKUKURU serikali imechukua hatua za kutengua uteuzi wa huyo Kaimu Afisa Mtendaji Mkuu na Bodi yake kwa kushindwa kuchukua hatua stahiki ili kuunusuru mradi mapema," amesema Eng. Kamwelwe.

Taarifa hizi zinaonyesha pamoja na mambo mengine udanganyifu uliofanyika kuhusu idadi ya visima vilivyokamilika kama ambavyo zimewasilishwa wizarani na DAWASA na uhalisia katika eneo la utekelezaji wa mradi.

Aidha Waziri Eng. Kamwelwe amemteua Dkt. Sufian Masasi kukaimu nafasi hiyo mpaka utaratibu mwingine utakapokamilika.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...