Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi alisema uagizaji wa baadhi ya bidhaa zikiwamo za chakula na Matunda nje ya Zanzibar umepungua kutokana na hamasa kubwa walionayo wananchi hasa wakulima katika muelekeo wa kuwekeza zaidi kwenye sekta ya Kilimo.
Alisema Sekta ya Kilimo ni miongozi mwa maeneo yaliyopewa kipaumbele cha kwanza na Chama Cha Mapinduzi wakati kilipoomba ridhaa ya kutaka kuongoza Dola kwenye kampeni za uchaguzi mkuu kilipokuwa kikitangaza Sera na Ilani yake.
Balozi Seif Ali Iddi alitoa kuli hiyo wakati alipofanya mahojiano maalum na Timu ya Wanahabari wa Redio Uhuru pamoja na Magazeti ya Chama cha Mapinduzi ya Uhuru na Mzalendo waliotaka kujua utekelezaji wa Ilani ya CCM kwa upande wa Zanzibar kwenye Ofisi ya Uratibu ya Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar Jijini Dar es salaam.
Alisema kutokana na Serikali za CCM kusamehe ushuru wa forodha kwa vifaa vya kilimo vinavyoingizwa nchini sambamba na kuendeleza mafunzo ya kisasa kwa wadau wa kilimo, wakulima wengi nchini hasa wale wanaojishughulisha na kilimo cha matunda wameongeza mara dufu uwezo wa uzalishaji.
Balozi Seif alisema katika kipindi cha miaka mitatu iliyopita mara baada ya kumalizika kwa uchaguzi mkuu wakulima wengi wamekuwa wakilalamikia ufinyu za soko la bidhaa wanazozalisha jambo ambalo limefikisha baadhi ya bidhaa hizo kusafirishwa kupelekwa upande wa Tanzania Bara.
Alisema hatua hiyo imeonyesha mabadiliko makubwa yaliyokuwa yamezoelekea kwa muda mrefu katika kushuhudia bidhaa nyingi hasa zile za nafaka, mizizi, mboga mboga pamoja na matunda ziliingizwa Zanzibar zikitokea mikoa mbalimbali ya Tanzania Bara.
Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar alisisitiza kwamba kwa vile kilimo ndio uti wa mgongo wa Taifa, Wananchi na hasa Wakulima wanapaswa kuendelea kuzalisha mazao yao katika kiwango kinachokubalika kitaalamu ili Taifa liendelee kupunguza kasi ya kuagiza bidhaa kutoka nje ya nchi.
Makamu
wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi kati kati akifanya
mahojiano maalum na Wanahabari wa Redio Uhuru pamoja na Magazeti ya
Chama cha Mapinduzi ya Uhuru na Mzalendo waliotaka kujua utekelezaji wa
ilani ya CCM kwa upande wa Zanzibar kwenye Ofisi ya uratibu ya Serikali
ya Mapinduzi ya Zanzibar (SMZ) Jijini Dar es salaam.
Balozi
Seif Ali Iddi akizungumza na Mkurugenzi wa Idara ya Asia wa Wizara ya
Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Bibi Justa Matari
Nyange Ofisi ya Uratibu wa SMZ Jijini Dar es salaam. Mazungumzo hayo
yalijikita katika kuangalia hatua zinazoendelea katika maandalizi ya
Ushiriki wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania katika Maonyesho ya
Kimataifa ya Biashara yanayotarajiwa kufanyika katika Jimbo la Guangzhou
Nchini China mnamo Mwezi wa Septemba Mwaka huu.
KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA
KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...