JOSEPH MPANGALA, MTWARA 

Mamlaka ya mapato mkoani Mtwara wamefanya ziara ya kushtukiza katika baadhi ya maduka kukagua mashine za kutolea risiti na kujionea kama wafanyabiashara wanatoa risiti lakii pia kama wateja nao wanadai risiti baada ya kufanya manunuzi.

Operesheni hiyo ambayo imeongozwa na kamishna msaidizi wa kodi za ndani operesheni ,Abdul Zuberi wamefanya ukaguzi katika maduka mbalimbali na kutoa elimu kwa baadhi ya wateja waliokuwa wakifanya manunuzi.

Zuberi amesema zipo changamoto ambazo zimekuwa zikilalamikiwa na baadhi ya wafanyabiashara ikiwemo mashine hizo kusumbua katika utoaji wa risiti

Pia amewataka wafanyabiashara ambao mashine zao zinapowasumbua kuwasiliana na wasambazaji wake na pindi wakikosa ushirikiano waende TRA kwa ajili ya ufumbuzi kwani mashine hizo zinakuwa hazina tatizo.

“Mkiona hampati huduma nzuri kutoka kwa wasambazaji mje TRA, kuna bwana mmoja alikuwa analalamikia mashine yake lakini kupata ushirikiano kutoka kwa msambazaji tumefika tumekuta ile mashine haina tatizo,”amesema Zuberi.
Kaim Kamishna wa Kodi za Ndani Operesheni Abdul Zuberi wakiwa na Meneja wa Kodi TRA Lucas Igembe Wakijadiliana Jambo mara baada ya kumaliza Ziara ya Kutembelea Maduka ya wafanyabishara kwa lengo la Kuhakiki Utumiaji wa Mashine za EFD Mkoani Mtwara.
Kaim kamishna waKodi za ndani Operesheni Abdul Zuberi akimsikiliza Mkurugenzi Mkuu wa Duka la uzwaji wa Vipuli la Prashant Mkoani Mtwara Sunil Janaksihn Gandhi wakati akitoa maelezo juu ya Utoaji wa risiti kwa wateja wake Mkoani Mtwara.
Mfanyabishara wa uuzaji wa Duka Kubwa {Supermarket} Dickson Mroso akitoa maelezo jinsi ya Utoani wa risisti kwa Wateja kwa Kutumia Mashine ya EFD kwa Kaim kamishna wa Kodi za Ndani Operesheni Abdul Zuberi mara baada ya Kutembelea katika Duka Hilo kwa Lengo la kutazama Matumizi sahihi ya Risisiti Mkoani Mtwara. 
Lucas Igembe Afisa Kodi TRA akihakiki Utoaji wa Risisti Uliotolewa kuanzia mwezi Juni kwa Kutumia mashine za EFD katika Duka Kubwa,Pembeni yake ni Meneja wa duka Hilo Dickson mroso. 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...