Na
Bashir Yakub.
Wapo watumishi wa umma ambao wameachishwa kazi kwasababu
mbalimbali na wanahisi kuwa pengine haki haikutendeka lakini hawajui la
kufanya. Basi waelewe la kufanya lipo na ni rufaa.
Na wengine wanajua kuwa ni
rufaa yumkini wasijue rufaa yenyewe inakatwa kwa utaratibu upi. Nitaeleza hapa,
lakini kwanza tujue nani mtumishi wa umma anayeongelewa hapa.
1.NANI MTUMISHI WA
UMMA.
Sheria namba 8 ya 2002, Sheria ya Utumishi wa Umma ,
iliyofanyiwa marekebisho na Sheria Namba 18 ya 2007 imemueleza mtumishi wa umma. Kifungu
cha 3
kinasema kuwa mtumishi wa umma ni yule anayefanya kazi katika ofisi
yoyote ya umma. Ili uelewe vizuri mtumishi wa umma anayeongelewa katika sheria
hii na katika makala haya ni yule
mfanyakazi/mwajiriwa wa serikali.
Kwahiyo watumishi wa bunge, maafisa wa mahakama, na wafanyakazi wa
taasisi/kampuni binafsi taratibu hizi za
rufaa zinazoelezwa humu haziwahusu.
Tunaongelea watumishi wa serikali kuu, za mitaa, mashirika ya
umma, idara na taasisi zote zilizopo chini ya serikali tukiondoa wale wa uteuzi
japo nao wanaongozwa na sheria hii.
2. HAKI YA RUFAA.
Unapokuwa umesimamishwa kazi rufaa ni haki yako ewe mtumishi.
Rufaa sio kuonesha ukorofi, sio kuwa mjuaji, sio kupingana na serikali, na sio
kukosa utiifu. Rufaa ni haki kama zilivyo haki nyingine za mshahara, likizo,
nk. Usiogope kukata rufaa kwani hata huyo aliyekusimamisha kazi naye
akisimamishwa anakata rufaa.
Kifungu cha 25( 1 ) (b) cha Sheria ya utumishi wa umma ndicho
kinachoeleza haki hii. Kadhalika kwenye barua yako ya kuachishwa kazi au siku ya kusimamishwa, yafaa na ni haki
uelezwe haki hii ya rufaa.
KUSOMA ZAIDI
sheriayakub.blogspot.com



Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...