WANAFUNZI wa chuo cha Mtakatifu Augustino cha jijini Mwanza(SAUT) wa mwaka wa kwanza na wapili wanaosoma kozi ya mawasiliano ya umma watembelea kituo cha kumbukumbu na Makaburi ya halaiki ya wahanga wa mauaji ya Kimbari Kigali nchini Rwanda.

Kituo hicho ambacho kimebeba historia ya nchi ya Rwanda pamoja na baadhi kumbukumbu ya vitu mbalimbali vya watu wa nchi ya Rwanda kabla na baada ya mauaji ya kimbari.

Baadhi Kumbukumbu zilizopo katika jengo la kumbukumbu ni picha za watu waliofariki dunia pamoja na picha za watoto ambao waliuwawa bila hatia yoyote mauaji na makaburi yalitokea Aprili 7, 1994.

Ambapo watu zaidi lakimbili na elfu hamsini walifariki dunia katika  Mauaji hayo kimbari nchini Rwanda.

Pia katika ziara hiyo wanafunzi wa chuo cha MT. Augustino walitembelea televisheni ya Taifa ya Rwanda, Rwanda Bordicasting Agency (RBA) na kujifunza vitu mbalimbali katika shirika hilo la utangazaji nchini Rwanda.
Lango la kuingilia katika makumbusho na Makaburi ya mauji ya kimbari Kigari nchini Rwanda. Baadhi ya Wananfunzi wa chuo cha Mtakatifu Augustino Mwanza wakiingia katika eneo la kumbukumbu.
 Mmoja wa wafanyakazi wa kituo cha kumbukumbu ya makaburi ya mauaji ya kimbari, Kazinimana Pacifique akizungumza na wanafunzi wa chuo kikuu cha MT Augustino jijini Mwanza mara baada ya kufika katika kituo cha kumbukumbu na makaburi ya pamoja ya mauaji ya Kimbari ambayo walitokea nchini Rwanda Mwaka 1994 ambapo mpaka kwaka huu 2018 wametimiza miaka 24 ya kumbukumbu ya mauaji hayo.Kushoto ni Mkuu wa kitengo cha Mawasiliano wa Chuo cha Mtakatifu Augustino(HOD), Peter Mwidima.
 Baadhi ya wanafunzi wa chuo cha Mtakatifu Austine wakiingia  katika chumba cha kuangalia moja ya sinema.
  Baadhi ya wanafunzi wanafunzi wakipiga picha nje ya Jengo ambalo limebeba historia ya nchi ya Rwanda pamoja na picha za wahanga wa mauaji ya kimbari na vitu mbalimbali ambavyo vimehifadhiwa humo.
 Moja ya kaburi la pamoja la wahanga wa mauaji ya Kimbari Kigari nchini Rwanda.
Wanafunzi wa chuo cha Mt. Augustino jijini Mwanza wakiwa katika picha ya pamoja na Mhariri mkuu Mtendaji wa Kituo cha Utangazaji cha Rwanda Broadcasting Agency. na Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano cha chuo cha Mtakatifu Augustino,(HOD), Peter Mwidima. 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...