Na Agness Francis,Globu ya Jamii

WAKAZI wa kijiji cha Mipeko katika Halmashauri ya Mkuranga mkoani Pwani  wameishukuru Serikali kuanza ujenzi wa vivuko katika mto Mzinga.

Akizungumza leo, Mkazi wa Kijiji cha Mipeko Fidelis Augustino ameishukuru Serikali kuwakumbuka kwa kuweka njia mbadala ili  kuwaondosha katika  janga hilo ambalo wananchi wanapata shida katika suala zima la uvukaji.

"Nina miaka zaidi ya miaka10 tangu nihamie huku, maji yamekuwa yakitusumbua kwa muda mrefu na  tulishindwa kupata ufumbuzi wa changamoto hii,"amesema.

Ujenzi huo una thamani ya Sh.bilioni 1.5 na tayari umeanza  kutekelezwa kujengwa kwa madaraja 3 katika vijiji vya  Kifaurongo, Mipeko na Tambani.
 Mkazi wa Kijiji cha Mipeko,Fidelis Augustino akizungumza na Globu ya jamii  kuwaomba wananchi wa kijiji hicho kuitunza miundo mboni ya madaraja yanayo njengwa.(Picha na Emmanuel Massaka,Globu ya jamii)
 Wananichi wa kijiji cha Kifaurongo wakivuka mto Mzinga kwa kutumia kivuko kinachovutwa  na vijana wanaojipatia kipato kwa kutoza shilingi mia 500/= kwa kila mtu mmoja, ambapo wanafunzi huwavusha kwa Shilingi mia 200/=.
Wananichi wa Kijiji  Mipeko wakivuka mto Mzinga sememu ambayo ujenzi wa Daraja umeaza.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...