Na Agness Francis,Globu ya Jamii
WAKAZI wa kijiji cha Mipeko katika Halmashauri ya Mkuranga mkoani Pwani wameishukuru Serikali kuanza ujenzi wa vivuko katika mto Mzinga.
Akizungumza leo, Mkazi wa Kijiji cha Mipeko Fidelis Augustino ameishukuru Serikali kuwakumbuka kwa kuweka njia mbadala ili kuwaondosha katika janga hilo ambalo wananchi wanapata shida katika suala zima la uvukaji.
"Nina miaka zaidi ya miaka10 tangu nihamie huku, maji yamekuwa yakitusumbua kwa muda mrefu na tulishindwa kupata ufumbuzi wa changamoto hii,"amesema.
Ujenzi huo una thamani ya Sh.bilioni 1.5 na tayari umeanza kutekelezwa kujengwa kwa madaraja 3 katika vijiji vya Kifaurongo, Mipeko na Tambani.
Mkazi wa Kijiji cha Mipeko,Fidelis Augustino akizungumza na Globu ya jamii kuwaomba wananchi wa kijiji hicho kuitunza miundo mboni ya madaraja yanayo njengwa.(Picha na Emmanuel Massaka,Globu ya jamii)
Wananichi wa kijiji cha Kifaurongo wakivuka mto Mzinga kwa kutumia kivuko kinachovutwa na vijana wanaojipatia kipato kwa kutoza shilingi mia 500/= kwa kila mtu mmoja, ambapo wanafunzi huwavusha kwa Shilingi mia 200/=.
Wananichi wa Kijiji Mipeko wakivuka mto Mzinga sememu ambayo ujenzi wa Daraja umeaza.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...