Mjumbe wa Kamati Kuu ya CCM, Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan leo ameongoza kikao Cha Kamati Maalum ya Halmashauri Kuu ya CCM Zanzibar katika ukumbi wa mikutano Afisi Kuu CCM Zanzibar.
Kikao hicho kilichobeba ajenda kuu mbili, ambazo ni Mapendekezo ya Kupiga Kura za maoni katika uchaguzi wa Jimbo la Jang’ombe na Mapendekezo ya Wanachama wa CCM wanao omba kuteuliwa kugombea nafasi ya Uwakilishi jimbo la Jang’ombe.
Mwenyekiti wa Kamati Maalum ya Halmashauri Kuu ya CCM Dkt. Ali Mohammed Shein yupo safarini nje ya nchi hivyo wajumbe walimchagua Mjumbe wa Kamati Kuu ya CCM, Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan kuwa Mwenyekiti wa muda na kuongoza kikao hicho.

 Mjumbe wa Kamati Kuu ya CCM, Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akiongoza kikao cha Kamati Maalum ya Halmashauri Kuu ya CCM Zanzibar kwenye ukumbi wa Afisi Kuu Zanzibar, kushoto ni Makamu wa Pili wa Rais Zanzibar Mhe.Balozi Seif Idd na kulia ni Naibu Katibu Mkuu wa CCM Zanzibar Dkt. Abdalla Juma Sadalla. (Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais)
 Mjumbe wa Kamati Kuu ya CCM, Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akisoma Ilani ya Uchaguzi ya CCM wakati kikao cha Kamati Maalum ya Halmashauri Kuu ya CCM Zanzibar kwenye ukumbi wa Afisi Kuu CCM Zanzibar, kushoto ni Makamu wa Pili wa Rais Zanzibar Mhe.Balozi Seif Idd
 Naibu Katibu Mkuu wa CCM Zanzibar Dkt. Abdalla Juma Sadalla akisoma ajenda zitakazojadiliwa kwenye Kikao cha Kamati Maalum ya Halmashauri Kuu ya CCM Zanzibar. 
 Wajumbe waliohudhuria Kikao cha Kamati Maalum ya Halmashauri Kuu ya CCM Zanzibar. (Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais)

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...