Na Ripota Wetu, Arusha
MAMLAKA
ya Hifadhi ya Ngorongoro (NCAA), imeanza kutekeleza mkakati wa
kushirikishana na wawekezaji waliopo sekta ya utalii ili kubaini maeneo
mapya yanayofaa kwa uwekezaji kwenye hifadhi hiyo.
Wajumbe
wa Menejimenti ya NCAA wamefanya ziara ya kutembelea maeneo hayo
yanayofaa kuwa uwekezaji katika huduma tofauti ikiwamo hoteli, kambi,
utalii wa magari ya waya maeneo ya bonde la Ngorongoro na Embakai.
Chini
ya uratibu wa Mpango wa matumizi bora (GMP), imeelezwa kwamba maeneo
haya yataongeza makusanyo ya mapato kutokana na shughuli za utalii
kwenye mamlaka ya hifadhi hiyo.
Akizungumza
kwenye ziara hiyo Naibu Mhifadhi wa mamlaka hiyo Asangye Bangu alisema,
ziara hiyo imelenga kuangalia maeneo yanayofaa kwa uwekezaji kama
hoteli,kambi za muda za kulala wageni ,utalii wa baluni na biashara
nyingine ndani ya hifadhi ikiwamo kuhakikisha wanakuwa na mpango
endelevu wa uhifadhi,utalii na jamii inanufaika
Naibu Mhifadhi wa Mamlaka ya Hifadhi ya Bonde la Ngorongoro Asangye Bangu akizungumza na wafanyabiahara wawekezaji waliofanya ziara ya kujionea maeneo mapya ya uwekezaji kwenye hifadhi hiyo.
Naibu Mhifadhi wa Mamlaka ya Hifadhi ya Bonde la Ngorongoro (NCAA) Asangye Bangu kulia, akizungumza na wafanyabiahara wawekezaji waliofanya ziara ya kujionea maeneo mapya ya uwekezaji kwenye hifadhi hiyo.
Wawekezaji na baadhi ya wafanyakazi wa Hifadhi ya Ngorongoro wakijadiliana baadhi ya masuala ya utalii pembeni mwa kivutio cha mwamba wa Nasera Rock kinavyopatikani hifadhin humo.
Mwenyekiti wa Chama cha Mawakala wa Utalii nchini (TATO), Wilbard Chambulo akiwaonyesha wawekezaji wenzake pamoja na maofisa wa Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro baadhi ya maeneo yanayozunguka kivutio cha Nasera Rock.
Baadhi ya wawekezaji waliotembelea Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro wakimsikiliza Naibu Mhifadhji Asangye Bangu.
KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA
KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...