Na Ripota Wetu, Arusha 
MAMLAKA ya Hifadhi ya Ngorongoro (NCAA), imeanza kutekeleza mkakati wa kushirikishana na wawekezaji waliopo sekta ya utalii ili kubaini maeneo mapya yanayofaa kwa uwekezaji kwenye hifadhi hiyo.

Wajumbe wa Menejimenti ya NCAA wamefanya ziara ya kutembelea maeneo hayo yanayofaa kuwa uwekezaji katika huduma tofauti ikiwamo hoteli, kambi, utalii wa magari ya waya maeneo ya bonde la Ngorongoro na Embakai.

Chini ya uratibu wa Mpango wa matumizi bora (GMP), imeelezwa kwamba maeneo haya yataongeza makusanyo ya mapato kutokana na shughuli za utalii kwenye mamlaka ya hifadhi hiyo.

Akizungumza kwenye ziara hiyo Naibu Mhifadhi wa mamlaka hiyo Asangye Bangu alisema, ziara hiyo imelenga kuangalia maeneo yanayofaa kwa uwekezaji  kama hoteli,kambi za muda za kulala wageni ,utalii wa baluni na biashara nyingine ndani ya hifadhi ikiwamo kuhakikisha wanakuwa na mpango endelevu wa uhifadhi,utalii na jamii inanufaika
 Naibu Mhifadhi wa Mamlaka ya Hifadhi ya Bonde la Ngorongoro Asangye Bangu akizungumza na wafanyabiahara wawekezaji waliofanya ziara ya kujionea maeneo mapya ya uwekezaji kwenye hifadhi hiyo. 
 Naibu Mhifadhi wa Mamlaka ya Hifadhi ya Bonde la Ngorongoro (NCAA) Asangye Bangu kulia, akizungumza na wafanyabiahara wawekezaji waliofanya ziara ya kujionea maeneo mapya ya uwekezaji kwenye hifadhi hiyo.  
 Wawekezaji na baadhi ya wafanyakazi wa Hifadhi ya Ngorongoro wakijadiliana baadhi ya masuala ya utalii pembeni mwa kivutio cha mwamba wa Nasera Rock kinavyopatikani hifadhin humo.
 Mwenyekiti wa Chama cha Mawakala wa Utalii nchini (TATO), Wilbard Chambulo akiwaonyesha wawekezaji wenzake pamoja na maofisa wa Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro baadhi ya maeneo yanayozunguka kivutio cha Nasera Rock.
 Baadhi ya wawekezaji waliotembelea Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro wakimsikiliza Naibu Mhifadhji Asangye Bangu.

KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...