Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Kangi Lugola akizungumza katika kikao chake na Maafisa Waandamizi wa Idara ya Uhamiaji kuhusu utaratibu wa kuunganisha mifumo ya vibali vya kazi na ukaazi. Kulia ni Kaimu Kamishna wa Vibali vya Ukaazi, Idara ya Uhamiaji, Mary Palmer, kushoto ni Afisa wa Kitengo cha Vibali vya Ukaazi, Isaac Fota, pamoja na Afisa Mahafudhi Nassoro. Kikao hicho kilifanyika katika Ukumbi wa Mikutano wa Wizara hiyo, jijini Dodoma leo, kabla ya kikao chake na Waziri wa Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Walemavu, Jenista Mhagama.  
 Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Kangi Lugola (kushoto meza kuu), akimsikiliza Waziri wa Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Walemavu, Jenista Mhagama alipokua akifafanua jambo kuhusiana na mfumo unaoziunganisha Wizara hizo mbili, wa utoaji wa vibali vya kazi na ukaazi. Kikao hicho kilifanyika katika Ukumbi wa Mikutano wa Wizara ya Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Walemavu, jijini Dodoma leo.  Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.   
 Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Kangi Lugola akizungumza katika kikao cha kujadili mfumo wa pamoja wa utoaji wa vibali vya kazi na ukaazi. Kulia meza kuu ni Waziri wa Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Walemavu, Jenista Mhagama. Mfumo huo unaoziunganisha wizara hizo mbili. Kikao hicho kilifanyika katika Ukumbi wa Mikutano wa Wizara ya wa Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Walemavu, jijini Dodoma leo.  

Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Kangi Lugola akiwa ofisini kwake jijini Dodoma mara baada ya kuwasili jijini humo leo. Waziri Lugola alifanya kikao na Maafisa Uhamiaji kutoka Kitengo cha Vibali vya Ukaazi, na baadaye alifanya kikao na Waziri wa Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Walemavu, Jenista Mhagama jijini humo, wakijadili mfumo wa pamoja wa utoaji wa vibali vya kazi na ukaazi ambao unaziunganisha Wizara hizo mbili.  

 Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Kangi Lugola (kushoto), akikaribishwa na Waziri wa Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Walemavu, Jenista Mhagama, ofisini kwake jijini Dodoma, kabla ya Mawaziri hao kuanza kikao cha kujadili mfumo wa pamoja wa utoaji wa vibali vya kazi na ukaazi ambao unaunganisha wizara hizo mbili. Kikao hicho kilifanyika katika ukumbi wa mikutano wa Wizara ya wa Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Walemavu, jijini humo leo. 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...