"Huyu binti anaitwa Theresia yupo hapa Mbulu, aliugua ghafla na kupooza upande wa kulia toka 2011,alikuwa hawezi kuongea kabisa kwa zaidi ya mwaka mmoja,baada ya matibabu kwa mwaka mmoja alianza kuongea kidogo na kukaa,

Lakini kutokana na hali kuwa ngumu ya kumuhudumia ,wazazi wake walishindwa kuendelea na matibabu,na kwa zaidi ya miaka sita amekuwa akilala ndani tu muda wote,na hawezi kufanya chochote japo kuwa kwa sasa anaweza kuongea kidogo saana na kwa mbali ananyanyua mkono wake,tumemtembelea na kumpatia kiti cha kumuwezesha hata kutoka nje. 

Tunatamani binti huyu aweze kuanza kupatiwa matibabu tena na mazoezi! Watanzania wenzangu tumsaidie, Tutawajulisha pindi tutakapojua taratibu zote za matibabu na gharama kisha tutatoa mawasiliano ya wazazi wake! Ana umri wa miaka 27 na kabla alikuwa ni mfanyakazi katika mamlaka ya maji safi Mbulu". 

Mungu Ibariki Tanzania

Taarifa hii ni kwa Hisani ya Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Mbulu Ndg. Hudson Kamoga

 Pichani ni  Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Mbulu Ndg. Hudson Kamoga akimsaidia  binti  Theresia mkazi wa Mbulu, kumtoa nje kwa njia ya baiskeli ya walemavu (Wheel Chair) ,Theresa aliugua ghafla na kupooza upande wa kulia tangu mwaka 2011,kufuatia hali hiyo bint huyo anahitaji msaada wa Matibabu

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...