Mwili wa Marehemu Msemaji wa Wizara ya Viwanda, Shadrack Sagati sasa utaagwa kwenye viwanja vya Mnazi Mmoja Jijini Dar es Salaam leo kuanzia saa 7 mchana hadi saa 11 jioni. 


Mabadiliko hayo yanafuatia kubadilika kwa njia zilizotumika kuusafirishia mwili huo kutokea mkoani Geita hadi Jijini Dar es Salaam,hivyo kusababisha kusogeza mbele kwa ratiba hiyo.

Kwa maana hiyo mabasi ya kuwachukua waombolezaji nyumbani kwa marehemu Kitunda Polisi, sasa yataondoka saa sita mchana, badala ya saa mbili asubuhi kama ilivyotangazwa hapo awali.

Hata hivyo kamati ya maandalizi pamoja na wahusika wote mnaombwa kuanza kuwasili uwanjani Mnazi mmoja saa 5 asubuhi.

Imetolewa na:
Kamati ya Maandalizi
Msiba wa Shadrack Sagati

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...