Na Stella Kalinga, Simiyu
Naibu Waziri wa Kilimo Dkt. Mwanjelwa ametoa wito kwa wakulima kote nchini kulima kilimo chenye tija kwa kutumia zana bora za kilimo ili kuongeza uzalishaji na kupata mavuno mengi na bora.

Dkt. Mwanjelwa ameyasema hayo Agosti Mosi, mara baada ya kukagua mabanda ya maonesho ya Kilimo katika Uwanja wa Nanenane wa Kanda ya Ziwa Mashariki uliopo Nyakabindi Bariadi, katika Maonesho ya Nanenane Kitaifa yanayofanyika Kitaifa Mkoani Simiyu.

Dkt. Mwanjelwa amesema Serikali kupitia Mfuko wa pembejeo unatoa mkopo wa pembejeo kwa riba ndogo sana, hivyo akatoa wito kwa wakulima wote nchini kwenda katika Halmashuri zao na kupata utaratibu wa kuomba mikopo hiyo ili waweze kupata mikopo itakayowawezesha kununua zana bora za kilimo.

“ Nitoe wito kwa wakulima wote nchini wajitahidi sana kwenda kwenye  kulima kilimo cha kisasa kilimo chenye tija, sisi kama Serikali tuna mfuko wetu wa pembejeo unaotoa mikopo kwa riba ndogo sana, hivyo wakulima wanaweza kuomba mikopo hiyo na kwenda kununua pembejeo bora za Kilimo” alisema Dkt. Mwanjelwa.

Katika hatua nyingine Dkt. Mwanjelwa amewataka maafisa ugani kuwafuata wakulima shambani badala ya kukaa ofisini, ili kuwapa elimu ya kilimo bora na kuwawezesha wakulima  kufikia lengo la kulima kilimo chenye tija.
Naibu Waziri wa Kilimo,  Mary Mwanjelwa  akikagua mashamba darasa ya JKT katika Uwanja wa Nanenane Nyakabindi Halmashauri ya  mji wa Bariadi leo Agosti Mosi, 2018, katika maonesho ya Nanenane Kitaifa mwaka 2018, Mkoani Simiyu.
Naibu Waziri wa Kilimo, Mary Mwanjelwa  akikagua mashamba darasa ya JKT katika Uwanja wa Nanenane Nyakabindi Halmashauri ya  mji wa Bariadi leo Agosti Mosi, 2018, katika maonesho ya Nanenane Kitaifa mwaka 2018, Mkoani Simiyu.
Mtaalam wa kutoka Jeshi la Magereza akitoa maelezo kwa Manaibu Waziri wa Kilimo, Dkt. Mary Mwanjelwa wakati walipotembelea mabanda ya maonesho ya mifugo ya Jeshi hilo katika Uwanja wa Nanenane Nyakabindi Halmashauri ya Mji Bariadi,  katika maonesho ya Nanenane Kitaifa mwaka 2018, Mkoani Simiyu.
Mtaalam wa Ufugaji wa Samaki kutoka JKT, Luteni Joseph  Lyakurwa(kulia) akitoa maelezo kwa   Manaibu Waziri wa Kilimo, Dkt. Mary Mwanjelwa (wa tatu kushoto)  na Omary Mgumba (kushoto) wakati walipotembelea mashamba darasa ya JKT katika Uwanja wa Nanenane Nyakabindi Halmashauri ya Mji Bariadi,  katika maonesho ya Nanenane Kitaifa mwaka 2018, Mkoani Simiyu.
Mtaalamu wa Jeshi la Magereza akitoa maelezo ya namna ya kutengeneza mkaa kwa kutumia mabaki ya mimea kwa   Manaibu Waziri wa Kilimo, Dkt. Mary Mwanjelwa (wa tatu kulia)  na Omary Mgumba (wa pili kulia) wakati walipotembelea mabanda ya maonesho ya Jeshi hilo katika  Uwanja wa Nanenane Nyakabindi Halmashauri ya Mji Bariadi,  katika maonesho ya Nanenane Kitaifa mwaka 2018, Mkoani Simiyu.
Naibu Waziri wa Kilimo, Mary Mwanjelwa akipewa maelezo kuhusu zana na mashine za kisasa  na wataalam wa JKT katika Uwanja wa Nanenane Nyakabindi Halmashauri ya Mji wa Bariadi leo Agosti Mosi, 2018, katika maonesho ya Nanenane Kitaifa mwaka 2018, Mkoani Simiyu.

KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...