VIONGOZI
wa shule mbalimbali nchini Tanzania wameshauriwa kuhakikisha
wanazifanya shule zao kuwa na mazingira salama, yenye utangamano,
ushirikiano, upendo pamoja na furaha kwa wanafunzi ili yaweze kumjenga
mtoto vema kielimu na maadili katika jamii.
Ushauri huo umetolewa jijini Dar es Salaam na Mkurugenzi Mtendaji wa Chama cha Waandishi wa Habari Wanawake Tanzania (TAMWA), Bi. Eda Sanga alipokuwa mgeni rasmi katika sherehe za Mahafali ya nane ya Darasa la Saba ya Shule ya Msingi St. Aloysius ya Mbezi Beach jijini Dar es Salaam.
Alisema shuleni, watoto wanapaswa kupewe ushauri nasihi na nasaha kadri inavyoitajika, huku wakiwa huru kutoa dukuduku zao na matatizo yao kwa walimu na kuyatatua kadri ya uwezo wao.
“Kuna kila sababu watoto kupewa ujuzi wa kutumia uwezo na mikono yao kufanya kazi na ujuzi wa kutumia akili zao za sasa kutatua migogoro yao kwa ngazi yao,” alisema Bi. Sanga katika hotuba yake.Aliwataka walimu mbali na kumjenga mwanafunzi kielimu kuna haja ya kuwaandaa pia kuwa wazalendo wa taifa lao na kikazi kinachojali wasionacho kama tunavyowajali watu walionacho.
“…Shule inatazamwa kama familia nje ya familia maana watoto wanatumia muda mwingi kuwa shuleni zaidi ya ule wawapo na familia zao nyumbani. Hofu ya Mungu ndio msingi wa mafanikio katika jambo lolote kwani inamjengea mtoto ujasiri, nidhamu na usubutu, naomba haya tuyazingatie pia.
Mkurugenzi Mtendaji wa Chama cha Waandishi wa Habari Wanawake Tanzania (TAMWA), Bi. Eda Sanga (kulia) na mgeni rasmi katika sherehe za Mahafali ya nane ya Darasa la Saba ya Shule ya Msingi St. Aloysius akimkabidhi cheti na zawadi mmoja ya wahitimu wa darasa la saba katika shule hiyo iliyopo Mbezi Beach Dar es Salaam.
Mkurugenzi Mtendaji wa Chama cha Waandishi wa Habari Wanawake Tanzania (TAMWA), Bi. Eda Sanga (kulia) na mgeni rasmi katika sherehe za Mahafali ya nane ya Darasa la Saba ya Shule ya Msingi St. Aloysius akimkabidhi cheti na zawadi mmoja ya wahitimu wa darasa la saba katika shule hiyo iliyopo Mbezi Beach Dar es Salaam.
Mwenyekiti wa Kamati ya Shule ya Msingi St. Aloysius, Kenneth Sinare (katikati) akimpongeza Mkurugenzi Mtendaji wa Chama cha Waandishi wa Habari Wanawake Tanzania (TAMWA), Bi. Eda Sanga (kulia) mara baada ya hotuba yake.
Mkurugenzi Mtendaji wa Chama cha Waandishi wa Habari Wanawake Tanzania (TAMWA), Bi. Eda Sanga na mgeni rasmi katika sherehe za Mahafali ya nane ya Darasa la Saba ya Shule ya Msingi St. Aloysius ya Mbezi Beach jijini Dar es Salaam akihutubia wanamahafali na wageni waalikwa.
Ushauri huo umetolewa jijini Dar es Salaam na Mkurugenzi Mtendaji wa Chama cha Waandishi wa Habari Wanawake Tanzania (TAMWA), Bi. Eda Sanga alipokuwa mgeni rasmi katika sherehe za Mahafali ya nane ya Darasa la Saba ya Shule ya Msingi St. Aloysius ya Mbezi Beach jijini Dar es Salaam.
Alisema shuleni, watoto wanapaswa kupewe ushauri nasihi na nasaha kadri inavyoitajika, huku wakiwa huru kutoa dukuduku zao na matatizo yao kwa walimu na kuyatatua kadri ya uwezo wao.
“Kuna kila sababu watoto kupewa ujuzi wa kutumia uwezo na mikono yao kufanya kazi na ujuzi wa kutumia akili zao za sasa kutatua migogoro yao kwa ngazi yao,” alisema Bi. Sanga katika hotuba yake.Aliwataka walimu mbali na kumjenga mwanafunzi kielimu kuna haja ya kuwaandaa pia kuwa wazalendo wa taifa lao na kikazi kinachojali wasionacho kama tunavyowajali watu walionacho.
“…Shule inatazamwa kama familia nje ya familia maana watoto wanatumia muda mwingi kuwa shuleni zaidi ya ule wawapo na familia zao nyumbani. Hofu ya Mungu ndio msingi wa mafanikio katika jambo lolote kwani inamjengea mtoto ujasiri, nidhamu na usubutu, naomba haya tuyazingatie pia.
Mkurugenzi Mtendaji wa Chama cha Waandishi wa Habari Wanawake Tanzania (TAMWA), Bi. Eda Sanga (kulia) na mgeni rasmi katika sherehe za Mahafali ya nane ya Darasa la Saba ya Shule ya Msingi St. Aloysius akimkabidhi cheti na zawadi mmoja ya wahitimu wa darasa la saba katika shule hiyo iliyopo Mbezi Beach Dar es Salaam.
Mkurugenzi Mtendaji wa Chama cha Waandishi wa Habari Wanawake Tanzania (TAMWA), Bi. Eda Sanga (kulia) na mgeni rasmi katika sherehe za Mahafali ya nane ya Darasa la Saba ya Shule ya Msingi St. Aloysius akimkabidhi cheti na zawadi mmoja ya wahitimu wa darasa la saba katika shule hiyo iliyopo Mbezi Beach Dar es Salaam.
Mwenyekiti wa Kamati ya Shule ya Msingi St. Aloysius, Kenneth Sinare (katikati) akimpongeza Mkurugenzi Mtendaji wa Chama cha Waandishi wa Habari Wanawake Tanzania (TAMWA), Bi. Eda Sanga (kulia) mara baada ya hotuba yake.
Mkurugenzi Mtendaji wa Chama cha Waandishi wa Habari Wanawake Tanzania (TAMWA), Bi. Eda Sanga na mgeni rasmi katika sherehe za Mahafali ya nane ya Darasa la Saba ya Shule ya Msingi St. Aloysius ya Mbezi Beach jijini Dar es Salaam akihutubia wanamahafali na wageni waalikwa.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...