UPANDE wa mashtaka katika kesi ya kugushi na utakatishaji wa fedha inayomkabili aliyekuwa Rais wa TFF Jamal Malinzi na wenzake wameiomba Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu kusimamisha ushahidi uliotolewa na Katibu Mkuu wa TFF, Wilfred Kidau ili waweze kumuita mtaalam wa Sayansi ya Tehama kutoa nyaraka za email alizozitoa katika kompyuta na kuchapisha(print).
Wakili wa Serikali kutoka Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa(Takukuru), Leornad Swai ameeleza hayo leo mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu, Wilbard Mashauri, kesi hiyo ilipopangwa kwa ajili ya kuendelea kusikilizwa kwa ushahidi wa Kidao.Swai amedai kesi hiyo ilipangwa kuendelea kusikilizwa, lakini imewapasa kumtumia Mtaalam wa Sayansi ya Tehama kwa kuwa yeye ndiyo aliyeta email katika kompyuta, kuichambua na kuichapisha (Print).
Na kuongeza kuwa wamefanya tafiti katika ushahidi wa vielelezo vya kielektloniki na kwamba ili kujenga msingi wa ushahidi wanaoutoa kutokana na maelekezo ya sheria ni vema wakasimamisha kwanza ushahidi uliopo ili mtu huyo aweze kutoa hizo nyaraka.Amedai kuwa, mtu huyo anauwezo wa kuitoa mahakamani kama sehemu ya kielelezo cha ushahidi na mashahidi wengine kuielezea.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...