Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Sera Bunge Kazi Vijana Ajira na Wenye Ulemavu Mhe. Jenista Mhagama ametembelea Idara na Vitengo vilivyopo Ofisi ya Waziri Mkuu Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu ili kujionea hali halisi ya utendaji kazi wa watumishi wa ofisi hiyo.
 Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Sera Bunge Kazi Vijana Ajira na Wenye Ulemavu Mhe. Jenista Mhagama akisisitiza jambo kwa afisa  wa hifadhi ya jamii wa Ofisi hiyo Bw. Saimon Mwanjala wakati alipotembelea Idara na Vitengo vilivyopo chini ya Ofisi ya Waziri Mkuu kuona utendaji wao leo jijini Dodoma. (Kushoto) Mkurugenzi wa Utawala na Rasilimali watu Bw. Peter Kalonga.
 Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Sera Bunge Kazi Vijana Ajira na Wenye Ulemavu Mhe. Jenista Mhagama akisalimiana na Mkurugenzi wa Sera na Mipango wa Ofisi ya Waziri Mkuu Kazi Vijana Ajira na Wenye Ulemavu Bw. Gabriel Saelie leo Jijini Dodoma wakati wa ziara yake ya kutembelea Idara na Vitengo vya Ofisi hiyo kujionea jinsi wanavyotekeleza majukumu yao.
 Mmoja wa watumishi wa Ofisi ya Waziri Mkuu Kazi Vijana Ajira na Wenye Ulemavu Bi. Leinila Mtilanjala akitoa maelezo kwa Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Sera Bunge Kazi Vijana Ajira na Wenye Ulemavu Mhe. Jenista Mhagama leo mjini Dodoma wakati alipotembelea Vitengo na Idara zilizopo chini ya Ofisi hiyo.
 Baadhi ya Watumishi wa Ofisi ya Waziri Mkuu Kazi Vijana Ajira na Wenye Ulemavu wakimsikiliza. Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Sera Bunge Kazi Vijana Ajira na Wenye Ulemavu Mhe. Jenista Mhagama (hayupo pichani) wakati wa ziara yake ya kutembelea Idara na Vitengo vya Ofisi hiyo kujionea jinsi wanavyotekeleza majukumu yao.

Mkurugenzi wa Utawala na Rasilimali watu Ofisi ya Waziri Mkuu Kazi Vijana Ajira na Wenye Ulemavu Bw. Peter Kalonga akimwelezea jambo kwa Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Sera Bunge Kazi Vijana Ajira na Wenye Ulemavu Mhe. Jenista Mhagama wakati wa ziara yake ya kutembelea Idara na Vitengo vilivyopo chini ya Ofisi hiyo. (Kulia) Mtakwimu Mwandamizi Idara ya Ajira Bw. Godwin Mpelumbe.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...