Waziri wa Madini na Mlezi wa Taasisi ya Doris Mollel, Angellah Kairuki (wa tatu kushoto), Mkuu wa Wilaya ya Same, Rosemary Senyamule (katikati) pamoja na Mkuu wa Idara ya Huduma za Kibenki kwa wateja binafsi wa benki ya CBA Tanzania, Julius Konyani (wa pili kushoto) wakiungana na watu wengine kumsikiliza Afisa Muuguzi Msaidizi wa Hospitali ya Wilaya ya Same, Entuja Mbwambo wakati akionyesha namna ya kutumia mashine maalum ya kumsaidia mtoto aliyezaliwa kabla ya wakati (Njiti) kupumua vilivyotolewa na Benki ya CBA Tanzania kwa kushirikiana na Taasisi ya Doris Mollel kwa hospitali hiyo, ambavyo thamani yake ni zaidi ya shilingi 20 milioni.
Waziri wa Madini na Mlezi wa Taasisi ya Doris Mollel, Angellah Kairuki pamoja na Mkuu wa Idara ya Huduma za Kibenki kwa wateja binafsi wa benki ya CBA Tanzania, Julius Konyani wakishirikiana kupanda mti katika eneo la Hospitali ya Wilaya ya Same, muda mfupi baada ya kukabidhi vifaa tiba vyenye thamani ya zaidi ya shilingi 20 milioni, vilivyotolewa na Benki ya CBA Tanzania kwa kushirikiana na Taasisi ya Doris Mollel kwa hospitali hiyo kwa ajili ya kusaidia watoto wanaozaliwa kabla ya wakati (Njiti).
Waziri wa Madini na Mlezi wa Taasisi ya Doris Mollel, Angellah Kairuki pamoja na Mkuu wa Idara ya Huduma za Kibenki kwa wateja binafsi wa benki ya CBA Tanzania, Julius Konyani  wakimsikiliza Mganga Mkuu wa wilaya ya Same, Dkt Godfrey Andrew wakati akifafanua jambo kuhusu vifaa vita alivyovipokea Hispitalini hapo, vilivyotolewa na Benki ya CBA Tanzania kwa kushirikiana na Taasisi ya Doris Mollel kwa ajili ya kusaidia watoto wanaozaliwa kabla ya wakati (Njiti).
Waziri wa Madini na Mlezi wa Taasisi ya Doris Mollel, Angellah Kairuki pamoja na Mkuu wa Idara ya Huduma za Kibenki kwa wateja binafsi wa benki ya CBA Tanzania, Julius Konyani, wakimjulia hali mtoto Amani John aliyelazwa katika wadi ya watoto ya Hospitali ya Wilaya ya Same, Mkoani Kilimanjaro aliyepata ajali ya kuungua na moto.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...