Na Chalila Kibuda, Globu ya Jamii
CHUO Kikuu Mzumbe kimesema kinaendelea kutoa elimu bora ikiwa ni katika kuendana na wakati ya kuhakikisha taaluma inayotolewa ni endelevu.

Hayo ameyasema Mkuu wa Tawi la Dar es Salaam Chuo Kikuu Mzumbe Profesa Honest Ngowi wakati akifungua mafunzo ya masuala ya usafrishaji na manunuzi kwa taasisi mbalimbali za ulinzi, mamlaka na Halmashauri katika kuhakikisha masuala ya usafirishaji na manunuzi yanaleta maendeleo.

Amesema mafunzo hayo yanafadhiliwa Taasisi ya Kuehne na kuendeshwa na  Chuo Kikuu Mzumbe amesema kuwa aliyeanzishwa taasisi hiyo amekuwa bilionea katika masuala ya usafirishaji na manunuzi ambapo ni kuhakikisha watu wanapata mbinu mpya za usafirishaji na manunuzi.

Mratibu wa mradi huo katika Chuo Kikuu Mzumbe Dk. Omary Swalehe amesema kuwa mradi huo ni wa miaka mitatu ambapo nia kutoa mafunzo kwa taasisi mbalimbali katika masuala ya usafirishaji na manunuzi.

Amesema kuwa hadi sasa wameshafanya katika awamu mbili ambapo katika maeneo tofauti ikiwa ni kuwajengea mbinu mpya za usafrishaji na manunuzi na kuweza kuona tija katika maendeleo ya nchi.
 Mkuu wa Chuo Kikuu Mzumbe Tawi la Dar es Salaam Profesa Honest Ngowi akizungumza katika ufunguzi wa mafunzo ya watu wa masuala ya usafirishaji na manunuzi wa taasisi za Serikali na Ulinzi katika Tawi hilo
 Mratibu wa mradi huo katika Chuo Kikuu Mzumbe Dk. Omary Swalehe akizungumza na waandishi habari kuhusiana na mradi wa masuala ya usafirishaji na manunuzi.

Baadhi ya wadau wakiwa katika mafunzo ya usafirishaji na manunuzi.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...