Na Karama Kenyunko, blogu ya jamii.

MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Kisutu imeamuru kumkamatwa kwa Mwenyekiti Wa Chadema Freeman Mbowe na Mbunge Wa Tarime Mjini, Esther Matiko ili waje kujieleza kwa nini wasifutiwe dhamana zao baada ya kukiuka masharti ya dhamana

Amri hiyo imetolewa leo Novemba 8.2018 na Hakimu Mkazi Mkuu Wilbard Mashauri wakati kesi hiyo ilipokuja kwa ajili ya washtakiwa kusomewa maelezo ya Awali (PH).

Akitoa uamuzi huo Hakimu Mashauri amesema, Novemba Mosi mwaka huu, Mdhamini wa mshtakiwa Mbowe, alifika mahakamani hapo na kudai kuwa, mshtakiwa amepelekwa South Afrika kutibiwa akiwa Mahututi na Mahakama iliamuru leo (siku ya kesi) alete taarifa kuhusu kuumwa kwake lakini hajaleta na badala yake amefika na kudai kuwa mshtakiwa yuko Dubai.

"Hii inaonesha kuwa, mdhamini huyu wa mshtakiwa Mbowe siyo muaminifu", amesema hakimu Mashauri.Pia kuhusu Mshtakiwa Matiko Hakimu Mashauri amesema kitendo cha mshtakiwa Matiko kusafiri nje ya nchi bila ridhaa ya Mahakama wala Polisi wanapotakiwa kuripoti kama masharti ya dhamana yanavyowataka ni matumizi mabaya ya haki yake ya dhamana.

Kutokana na sababu hizo mahakama inaamuru mshtakiwa Mbowe na Matiko wakamatwe na kufikishwa mahakamani hapo ili kujieleza kwanini wasifutiwe dhamana zao" amesema Mashauri.Awali kabla ya amri hiyo Wakili Nchimbi, alihoji kwanini  Mbowe na Matiko hawapo mahakamani.

Mdhamini wa Mbowe alisimama na kueieleza mahakama kwamba Mbowe yupo Dubai kwa ajili ya matibabu na hajawahi kusema kwamba yupo Afrika Kusini."Nimeongea naye moja kwa moja yupo nchini Dubai,"ameeleza.

KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA>>>>>

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...