Na Bashir
Yakub.
1.UKAZAJI WA HUKUMU NI
NINI.
Ukazaji wa hukumu ni hatua inayochukuliwa na mtu aliyeshinda
kesi/shauri kwa kuiomba mahakama kumlazimisha mtu aliyeshindwa katika
kesi/shauri kufanya au kutekeleza kile ilichoamua dhidi yake/mshindwa. Kawaida
mtu akishindwa kesi/shauri mahakama huwa inatoa maagizo mbalimbali. Mathalan,
agizo la kulipa hela, agizo la kurudisha nyumba au mali fulani, agizo la
kubomoa, agizo la kuondoka katika pango au katika nyumba,kiwanja fulani, agizo
la kujenga, agizo la kulipa fidia, faini, gharama n.k. Maagizo yako ya aina nyingi inategemea na shauri na
shauri.
Hivyo basi, ukazaji hukumu/utekelezaji huwa ni kulazimisha
agizo aumaagizo ya aina tuliyoona hapo
juu yaweze kutekelezwa kama ilivyoamriwa.
2. NI WAKATI GANI HUKUMU HUTAKIWA KUKAZWA.
Kwa ujumla mahakama inapotoa hukumu basi yule aliyeshindwa
mara moja au ndani ya muda aliopewa kama amepewa,hutakiwa kutekeleza kile
kilichoamuliwa kwa hiari yake. Aliyeshindwa akikataa kutekeleza kile
kilichoamuliwa kwa hiari yake basi ni wakati huu ambapo suala la kukaza/kutekeleza hukumu kwa njia
mahakama huja. Kwa maana nyingine mtu
aliyeshndwa akiamua kwa hiari yake kufanya yale aliyoagizwa na mahakama basi
suala ukazaji wa hukumu haliwezi kuwepo.
3. UMUHIMU WA KUZUIA HUKUMU KUKAZWA.
Sababu za msingi zinazoweza kupelekea kuzuia hukumu kukazwa
ni pamoja na sababu kuwa umekata rufaa na hivyo ukazaji wa hukumu usimame ili
rufaa yako isikilizwe kwanza, sababu nyingine ni iwapo kesi imeendeshwa bila
wewe kujua au kuwepo isipokuwa umeshtukia tu watu wanakuja kukaza hukumu,
sababu nyingine ni iwapo una maslahi
katika mali inayokaziwa hukumu kwa mfano ni mali ya ndoa na hukuwa na
taarifa na kilichoendelea, ni mali yako
lakini inataka kuuzwa au kutumika kutekeleza hukumu kwa kesi ambayo sio yako na
pengine hukuwahi kujua uwepo wake, nk.
KUSOMA ZAIDI
sheriayakub.blogspot.com
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...