Na  Bashir  Yakub.

1.UKAZAJI WA HUKUMU NI NINI.

Ukazaji wa hukumu ni hatua inayochukuliwa na mtu aliyeshinda kesi/shauri kwa kuiomba mahakama kumlazimisha mtu aliyeshindwa katika kesi/shauri kufanya au kutekeleza kile ilichoamua dhidi yake/mshindwa. Kawaida mtu akishindwa kesi/shauri mahakama huwa inatoa maagizo mbalimbali. Mathalan, agizo la kulipa hela, agizo la kurudisha nyumba au mali fulani, agizo la kubomoa, agizo la kuondoka katika pango au katika nyumba,kiwanja fulani, agizo la kujenga, agizo la kulipa fidia, faini, gharama n.k. Maagizo  yako ya aina nyingi inategemea na shauri na shauri.
Hivyo basi, ukazaji hukumu/utekelezaji huwa ni kulazimisha agizo aumaagizo  ya aina tuliyoona hapo juu yaweze kutekelezwa kama ilivyoamriwa.

2.  NI WAKATI GANI HUKUMU HUTAKIWA KUKAZWA.
Kwa ujumla mahakama inapotoa hukumu basi yule aliyeshindwa mara moja au ndani ya muda aliopewa kama amepewa,hutakiwa kutekeleza kile kilichoamuliwa kwa hiari yake. Aliyeshindwa akikataa kutekeleza kile kilichoamuliwa kwa hiari yake basi ni wakati huu ambapo  suala la kukaza/kutekeleza hukumu kwa njia mahakama huja.  Kwa maana nyingine mtu aliyeshndwa akiamua kwa hiari yake kufanya yale aliyoagizwa na mahakama basi suala ukazaji wa hukumu haliwezi kuwepo.

3. UMUHIMU WA  KUZUIA HUKUMU KUKAZWA.
Sababu za msingi zinazoweza kupelekea kuzuia hukumu kukazwa ni pamoja na sababu kuwa umekata rufaa na hivyo ukazaji wa hukumu usimame ili rufaa yako isikilizwe kwanza, sababu nyingine ni iwapo kesi imeendeshwa bila wewe kujua au kuwepo isipokuwa umeshtukia tu watu wanakuja kukaza hukumu, sababu nyingine ni iwapo una maslahi  katika mali inayokaziwa hukumu kwa mfano ni mali ya ndoa na hukuwa na taarifa na kilichoendelea,  ni mali yako lakini inataka kuuzwa au kutumika kutekeleza hukumu kwa kesi ambayo sio yako na pengine hukuwahi kujua uwepo wake, nk.
                  
KUSOMA  ZAIDI  sheriayakub.blogspot.com


Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...