*Viongozi wazungumzia ubora wa bidhaa zao, waipongeza Serikali
*Watakaonunua bidhaa kwao kuingia kwenye droo kila siku
Na Said Mwishehe,Globu ya jamii.
DUKA kubwa la kisasa linaouza bidhaa za aina mbalimbali za Samsung zenye viwango vya hali ya juu katika ubora limefunguliwa Posta katikati ya Jiji la Dar es Salaam.
Uzinduzi wa duka hilo umefanyika leo Desemba 24 mwaka 2018 ambapo viongozi wa ngazi mbalimbali wa kampuni ya Samsung ndani na nje ya Tanzania pamoja na baadhi ya wananchi wa Jiji hilo wameshuhudia uzinduzi huo uliokwenda sambamba na punguzo la bei pamoja na droo mbalimbali za kujishindia zawadi kwa wanaonunua bidhaa zao.
Akizungumza wakati wa uzinduzi wa duka hilo lililopo jengo la Askari Posta Mpya jijini Dar es salaam Mkurugenzi wa vifaa vya kieletroniki Happy Grayson amesema Samsung ni bidhaa kubwa duniani na yenye ubora wa uhakika.
“Tumeamua kufungua duka hili eneo la Posta mpya jijini Dar es Saam kwa ajili ya kuhakikisha bidhaa zetu zinapatikana kwa urahisi na gharama nafuu.Hatutaki watu wanaohitaji bidhaa za Sumsung wasumbuke kuzipata.
“Tunayo maduka mengi nchini ikiwemo jijini Dar es Saalam lakini umuhimu wa duka hili unatokana na ukweli kwamba kuna bidhaa zote za Samsung ambazo mteja anahitaji kununua kutoka kwetu,”amesema.
Mkurugenzi Mkuu wa Samsung Afrika Mashariki Hong Seok na Mkurugenzi wa vifaa vya kieletroniki Happy Grayson wakikata utepe wakati wa uzinduzi wa duka jipya la vifaa vya Samsung Posta jijini Dar es salaam leo kulia ni Abraham Okore Mkuu wa Usambazaji Samsung na kushoto ni Suleiman Mohammed Meneja Mkazi wa Samsung.
Mkurugenzi Mkuu wa Samsung Afrika Mashariki Hong Seok na Mkurugenzi wa vifaa vya kieletroniki Happy Grayson, , Abraham Okore Mkuu wa Usambazaji Samsung na Suleiman Mohammed Meneja Mkazi wa Samsung wakiingia dukani mara baada ya kukata utepe wakati wa uzinduzi huo.
Mkurugenzi Mkuu wa Samsung Afrika Mashariki Hong Seok akipata maelezo kutoka kwa Mkurugenzi wa vifaa vya kieletroniki Happy Graysonmara baada ya kuzinduliwa kwa duka hilo.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...