Na Mathias Canal-WK, Mtwara

Wakulima wa zao la korosho wa Wilaya ya Tandahimba na Masasi wamekubali kuuza korosho zao mbele ya Waziri wa kilimo Mhandisi Dkt Charles Tizeba (Mb) kutokana na kuridhia na kukubaliana na maamuzi ya serikali.

Hayo yamejili katika mnada wa nne wa msimu wa uuzaji korosho 2018/2019 uliojumuisha kampuni za ununuzi 11 katika maghala tofauti uliofanyika katika kijiji na kata ya Mdimba Mkoani Mtwara.

Akizungumza kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika katika kijiji na kata ya Mdimba, Waziri wa kilimo Mhandisi Dkt Charles Tizeba alisema kuwa bei ya zao la korosho imeonyesha mwelekeo wa kushuka katika mwaka 2018/2019 tofauti na hali ilivyokuwa katika msimu wa mwaka 2017/2018 ambapo bei ya zao hilo ilifikia shilindi 4,128

Katika mkutano huo wakulima wa korosho walikubali mbele ya waziri wa kilimo Mhandisi Dkt Tizeba kuanza kuuza korosho zao kwa bei ya juu ya shilingi 3,016 huku bei ya chini ikiwa ni shilingi 3000.

“Wafanyabiashara wasipangiwe muda wa kuchukua korosho ghalani kwa ajili ya usafirishaji na wasipangiwe kutumia bandari gani, wawe huru kulingana na maagizo yaliyotolewa na Rais Magufuli’’
Waziri wa kilimo Mhandisi Dkt Charles Tizeba (Mb) akizungumza na wananchi waliojitokeza kwenye mnada wanne wa msimu wa uuzaji korosho 2018/2019 wakati wa mkutano wa hadhara uliofanyika katika kijiji na kata ya Mdimba Mkoani Mtwara jana tarehe 2 Novemba 2018. (Picha Zote Na Mathias Canal, WK)
Baadhi ya wananchi waliojitokeza kwenye mnada wanne wa msimu wa uuzaji korosho 2018/2019 wakimsikiliza kwa makini waziri wa kilimo Mhandisi Dkt Charles Tizeba (Mb) akizungumza katika kijiji na kata ya Mdimba Mkoani Mtwara jana tarehe 2 Novemba 2018.
Waziri wa kilimo Mhandisi Dkt Charles Tizeba (Mb) akizungumza na wananchi waliojitokeza kwenye mnada wanne wa msimu wa uuzaji korosho 2018/2019 wakati wa mkutano wa hadhara uliofanyika katika kijiji na kata ya Mdimba Mkoani Mtwara jana tarehe 2 Novemba 2018.
Baadhi ya wananchi waliojitokeza kwenye mnada wanne wa msimu wa uuzaji korosho 2018/2019 wakimsikiliza kwa makini waziri wa kilimo Mhandisi Dkt Charles Tizeba (Mb) akizungumza katika kijiji na kata ya Mdimba Mkoani Mtwara jana tarehe 2 Novemba 2018.


Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...