Waziri wa Vijana,Utamaduni,Sanaa na Michezo wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar(SMZ) Balozi Ali Abeid Aman Karume amewataka Watanzania kutembelea sehemu za Vivutio vya Utalii na kuondokana na dhana kwamba utalii unafanywa na wageni tu.

Balozi Karume ameyasema hayo leo Wilayani Mbozi,Mkoa wa Songwe wakati alipotembelea eneo la urithi na uhifadhi ambapo kulidondoka KIMONDO chenye uzito wa tani 12 kinachokifanya KIMONDO hicho kinachopatikana Mkoa wa Songwe kuwa ni cha nane(8) duniani na cha pili Afrika kwa Uzito.

“Nimefurahishwa sana na Historia ya kimondo hichi,ni vyema Watanzania wengi zaidi wakatenga muda kuja kujifunza hapa.Ni jambo la kujivunia kidunia kuwa sehemu ya nchi zanye Vimondo vizito zaidi duniani”Alisema Balozi Karume.

Wakati huo huo Balozi Karume aliongozana na Mkuu wa Mkoa wa Songwe Brig. Jenarali Mwangela,*Naibu Waziri Mavunde* na Naibu waziri wa Vijana SMZ Mh Lulu Mshamu kukagua maandalizi ya mwisho ya Uzinduzi wa Mbio za Mwenge Kitaifa zinazotarajiwa kuzinduliwa tarehe 2.4.2019 Mkoani Songwe.






Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...