Mbunifu wa mavazi na mwanaharakati wa vijana kutoka Tanzania Rahma Bajun alipokea tuzo ya utambuzi kutoka kwa Rais wa Misri Abdelfattah Elsisi ambaye pia ni Mwenyekiti wa Kamisheni ya Umoja wa Afrika Moussa Faki.
Tuzo hiyo ilitolewa jijini Aswan nchini Misri kwenye mkutano wa “Arab and African Youth Platform” uliofanyika hivi karibuni Rahma sambamba na vijana wengine 9 kutoka nchi za Afrika na za Kiarabu wanaotoka kwene sekta mbalimbali wamepokea tuzo hizo za heshimwa kwa mchango wanaotoka vijana, nchi zao na Afrika kwa ujumla.
Rais wa Misri Abdelfattah Elsisi(Kushoto) akimkabidhi Mtanzania Bi. Rahma Bajun tuzo ya 'Most inspiring youth in Africa and Arab region' wakati wa mkutano wa Arab and African Youth Platform uliofanyika nchini Misri.
Mbunifu wa mavazi na mwanaharakati wa vijana kutoka Tanzania Rahma Bajun (wa tatu kutoka kushoto) akiwa pamoja na washiriki wengine kutoka Barani Africa wakati wa mkutano huo.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...